GILASI YA MWISHO MAKABURINI
Katika hadithi hii tunapatana na Msoi mwenye utambuzi wa kipekee ya mamabo
yatakayotokea. Msoi alipata hisia flani yenye kitisho na wasiwasi. Ndoto nyingi
ambazo Msoi aliwahi kuota mara mara hua ingawa marafiki wake hawakuamini.
Hisia hizo ambazo Msoi alijaribu kuepuka kwa
muda kwa mwezi mmoja hatimaye zilimfanya awe mwoga zaidi yeye pamoja na marafi zake walikuwa wanaenda katika bar
iliyokuwa kwenye maskani ya mava ili kunywa
na kujiburudisha baada ya kazi.
Pia pahali hapo palipopachikwa jina la kimombo exotic resort.
Siku moja aliamua kutoenda katika mava kwani
hisia zake zilimfanya aogope sana. Kwa sababu aliona kwamba balaa kubwa
itatokea,Semkwa rafikiye Msoi alienda kwake nyumbani ili kumsihi waende katika
mava akaitikia shingo upande. Walipokuwa wakitokea Msoi aliligonga bakuli la
maua likavunjika vipande vipande ,alikuwa karibu kuanguka akiteremsha mguu na
pia alijibana kidole kidogo kwenye
mlango wa gari. Hizi zilikuwa ishara za kuonyesha kwamba jambo mbaya
litatendeka.
Njiani walisikia mgurumo wa radi ambayo
Semkwa aliona kuwa jambo la kawaida. Walipofika kwenye daa ya makaburini,walipatana
na Asha na Josefina. Walipokaa
chini,Msoi aligeuza namna yake ya kukaa. Siku hiyo alitaka kuyaangalia mava ili jambo likitokea ataweza
kutoroka.
Muda ulivyozidi kuyoyoma , Msoi na marafiki
wake walijiburudisha na vinywaji na
muziki uliochezwa na bendi. Asha na Msoi
walipokuwa wakichheza densi, Msoi alionekana mwenye wasiwasi. Wenzake wakaanza
kumtani hadi ikambidi anyamaze ili angoje kile ambacho kitaendeea. Msoi alingwa
na kuburudika nao ijapokuwa walimtani na kumkejeli kuhusu ndoto zake. Asha aliburudishwa na Msoi
kuhusu matukio yaliyotendeka na Msoi
kuhusu matukio yaliyotendeka awali ambayo aliona kama ni ya bure tu. Msoi
aliamua kujinyamazia.
Wakati ambao
kila mtu alikuwa ameshiba walicheza mziki huku wakiwa kwani hawakutosheka.
Baada ya muda mfupi, Msoi aliviona vizuu vimejifufua kwa mtindo wa
Thriller wa Micheal Jackson, Asha
alipiga uyoe ambao uliskika na kila mtu. Watu walipoona yaliyokuwa yakiendelea
walitimua mbio hadi kwao nyumbani. Wengine walianguka na kukanyang’wa
Baada ya
Asha na Msoi kufika nyumbani waliskia habari kwenye televisheni kwamba wale
vizuu walikuwa majambazi ili waibie Baa ya Makaburini pamoja na wateja wao.kwa
mara nyingine marafiki zake Msoi walifahamishwa kwamba wanafaa kumsikiliza.
DHAMIRA.
Ø Mwandishi anatuhimiza tusipuuze mambo ambayo tunaonywa na marafiki zetu.
MAUDHUI
Ø
ANASA NA STAREHE
Tunaona kwamba Msoi na Asha walikuwa wanaenda kwenye
baa ya makaburini kujiburudisha baada ya kazi na kulewa kiasi cha kujisahau.
Ø
UHALIFU
Majambazi
walivamia watu na kuwaibia mali yao
kwani waligundua kwamba watu huogopa wafu
Ø
ITIKADI NA USHIRIKINA
Ushirikina ni ile hali ya kuamini nguvu nyingine kuliko mungu
Msoi
aliamini kwamba baa iliyokuwa kwenye mandhari ya mava ingevamiwa na watu
wasiojulikana
Ø
URAFIKI NA UTANGAMANO
Akina
Semkwa,Msoi,Asha na Josephina waliburudika pamoja na kutengamana.walifanya m
ambo pamoja
Ø
UWOGA
Msoi aliota
ndoto ambazo zilimfanya awe mwoga.
WAHUSIKA
1.Msoi.
Ni mtu
mwenye kipawa utambuzi wa mambo
SIFA
I.
Ni mbarazi ,ana mazoea ya kukaa na watu wengine hasa katika baa.
II.
Ni mshiriki anasa,amekuwa akizuru bar ya makaburini ili kustarehe.
III.
Ni mpole,hana mambo mengi.
IV.
Ni mwoga.
V.
Ni mshirikina,anaamini katika mambo ya ushirikina.
VI.
Anashawishika kwa urahisi.
2.Semkwa,Asha na Josefina.
I.
Ni
wabaraza
II.
Wapenda anasa,kila wikendi walikuwa wanakutana
katika baa na kuburudika pamoja.
III.
Wabishi,walibishana
na Msoi alipowadokezea kuhusu ndoto yao.
IV.
Weye
utani ,wanamtania Msoi anapowaeleza kuhusu ndoto yake.
3.Majambazi.
I.
Ni
watu wabunifu –walivaa kama wafu ili waweze kuwaogofya watu
II.
Ni
waoga-hawajitokezi moja kwa moja kukabiliana na watu.
III.
Wahalifu
–walijaribu mali ya watu baada ya kuwaibia.
KIKAZA.
Hadithi hii
inazungumzia kikaza ambacho ni suruali spesheli. Kikaza hiki kimetumiwa
kusimamia uongozi katika jamii. Kikaza ni jazanda inayosimamia uongozi. Hadithi inaanza pale ambapo kuna
dalili za mvua kunyesha,lakini Mzee Babu akawafahamisha wanakijiji kwamba
haitanyesha. Kwanza wanatekede hawakuamini. Kulikuwa na kikao kwa mzee huyu na
miongoni mwa waliohudhuria ni Bi Cherenga almaarufu Bi Cherehani na Bw Pima,Bw
Machupa pia alikuwepo(msemaji wa kijiji). Wote walitaka Mzee Babu awafunulie
kitendawili.
Washona
kikaza ni wananchi wenyewe. Kikaza kilikuwa kimepasuka. Bw Mtajika(kiongozi)
alifanya makosa kumwacha Bi Mtajika
kukiguza kikaza,kwani yeye siye kiongozi. Mapinduzi ni marekebisho yalihitaji
kufanywa. Kulikuwa nia uongozi mbays. Bw Pima alipima kikaza na Bi Cherehani
kukishona. Bi Cherehani aliwahimiza wanatekede
kwenda kukishona kikaza (kurekebisha makosa na kumtoa Bw Mtajika
mamlakani) . Kikaza kilihitaji kushonwa. Bi Cherehani alihakikisha kwamba atapunguza kipimo ili
kikaza kikaze. Kikaza (uongozi) ni cha ushirika.
DHAMIRA.
Mwandishi
anataka kuonyesha kwamba uongozi ni
ushirika.
MAUDHUI
1.UONGOZI
Hadithi hii inaongea kuhusu swala la uongozi.
·
Uongozi umewakilishawa na kikaza – “suruali ya ndani”
·
Uongozi
hushonwa na wananchi.
·
Uongozi
ni ushirika.
·
Uongozi
mzuri au mbaya hutokana na mchango wa watu wenyewe
·
Mwandishi
pia anaguzia swala la uongozi mbaya
·
Bw
Mtajika tunaelezwa kwamba kikaza chake kimeraruka na basi uongozi umeigiza
dosari.
·
Bi
Mtajika amechangia katika uongoza mbaya.
·
Wanawake walishona kikaza kiliochobana
2.UBINAFSI
Bw Mtajika
na wenzake waliochaguliwa waliochaguliwa waliwasahau waliwasahau wenzao waliowachagua kama vile
kobe alivyowatendea hadithi yake kuenda angani.
3.USHIRIKIANO
Kikaza
kilishonwa kwa kushirikiana. Katika uongozi, lazima pawepo na ushirikiano wa
watu wote.
4. MABADILIKO
Baada ya
mambo kugonga mwamba, viongozi wanatolewa mamlakani na kubadili uongozi.
5. USALITI
Bwana
mtajika na Bi. Mtajika , anawasaliti wananchi kwa kuongoza vibaya na kutomzuia
mkewe kukigusa kikaza.
6. UKARIMU
Babu na
wanakijiji ni wakarimu wanapopeana mavuno.
7. KUTOWAJIBIKA
Viongozi
hawakuajibika katika uongozi wao.
8. UTABIRI
Babu
anatabiri.
WAHUSIKA
1. MZEE BABU
·
Ni
mtabiri
·
Mkarimu
·
Mwenye
busara . Anawatetea na kuwashauri watu
·
Mbaraza.
Anapenda kuingiana na watu.
·
Mtambuzi
wa mambo.
2. BW. MTAJIKA
Kiongoziwa
tekede.
SIFA
1. Ni mweledi wa kuongea .anapoongea,
hawei kubadilisha ukweli kuwa uongo.
2. Mwenye ubinafsi. Alipopata cheo,
aliwasahau wengine.
3. Ni mwanamme anayetawaliwa na mkewe.
Alikua amezidiwa na nguvu za pili.
4. Msailiti. Amewasaliti wananchi wa
Tekede kwa kuwasahau (hadithi ya safar ya mzee kobe kwenda angani. )
3. BI CHEREHANI/ BI CHIRENGA.
·
Mshonaji
kikazi.
·
Ni
mnyamavu kwani hapendi kuzungumza
·
Ni
mwenye soni
·
Mkweli.
Hapiti njia mbili. Hafichi mambo.
·
Ni
mzalendo .hakwenda ikuliuni peke yake.
·
Mwenye
bidii kwani anashona kikaza kama jukumu lake.
·
Mvumilivu.
Amevumilia kukemewa na watu.
4. BI MTAJIKA.
Msaliti
anakigusa kikaza ingawa anaelewa itikada ya jamii ya wana Tekede inayosema
kwamba wa pili hafai kugusa kikaza.
Ni mkoloni
kwani anaamua kutawala watu apendavyo yeye.
5. WANAKIJIJI
Ni
wakarimu.Walimpa babu mavuno waliyoyapata.
Wenye
mapinduzi. Watu walizinduka kuhusu uongozina Bw. Mtajika.
Ni wenye
ushirikiano.Wanashirikiana kumtoa Bi Mtajika kwenye mamlaka.
Ni wasikivu.
Wanamsikiliza babu kwa makini.
Ni wenye
utamaduni.Wanatii tamaduni zao.K.m bibi hakustahili kugusa kikaza.
MBINU ZA LUGHA
a) TASHTITI
Ni mbinu ya
kukejeli mtu kwa njia ya kutomuudhi moja kwa moja.
Hadithi ya
kobe ni tashtiti murua inayoonyesha ubadhilifu, ukaidi na uogozi mbaya wa Bw.
Mtajika. Mzee Babu anawapa watu hadithi badala ya kusema yote aliyoyafanya
kombo Bw. Mtajikana adhabu atakayoipata atakaposhushwa madaraka.
Ushonaji wa
kikaza vibaya kwa Bi. Cherehani na Bw. Pima pia ni tashtiti. Yaonyesha namna
ambavyo wanakijiji wa Tedeke waliomchagua kiongozi aliyefaa.
Msemo wa
nyani haoni kundule ni semi linaloeleza upambano na kutojali kwa wanakijijij wa
Tekede.
b. FUMBO
Kikaza
kimetumika kimafumbo kumaanisha uongozi, upimaji Na kushonwa kwa kikaza ni
kumteua na kumtwika majukumu ya uongozi. Kupima na kushona kikaza ina maana ya
ushirikiano wa jamii katika kumchagua na kumsimika kiongozi.
Wa pili
hakuruhusiwa kushika kikaza ni mke wa kiongozi. Kutanda Kwa mawingu meusi
angani kusha kukosa kunyesha ni fumbo inayoeleza dhiki ya waakaazi wa Tekede.
c. HADITHI
Hadithi
katika hadithi hii inamhusu kobe inayosimuliwa na mzee Mzee Babu. Musiliko wa
karamu angani ilimjulisha kobe, ndege na kadhalika. Mzee kobe alifanya ujangili
na kudai jina sisi sote.
Kila
chakula, kinywaji na starehe zilielekezwa kwake. Ndege walitababika na kuamua
kumnyanyanya kobe. Manyoya yao na kobe hakuweza kupaa tena ndio maana gamba la
kobelena viraka au mipasuko.
D. MAJAZI
Mbinu za
kisanaa.
Baadhi ya
wahusika wanapewa majina kulingana na sifa au hulka zao. K.m. Mzee Babu alikuwa
mzee kuliko wengine. Bw. Mtajika alitojwa mara kwa mara na kila mtu kwa sababu
alikua kiongozi wao. Bw.Machupa pima aliyapima kwa uangalifu alivyowaambiwa
wanakijiji.
Bw Machupa
hakuwa na msimamo dhabiti hasa kuhusu uongozi wa Bw. Mtajika.
e. TAKRIRI
Baadhi ya kauli
zimekaririwa ili kutilia mawazo Fulani mkazo k.m Bw. Cherehani na Bw. Pima
walikuwepo kushiriki na kutoa mchango
walikuwepo vilevile.
Kitendawili
cha kukaza kikazidi kukazaa.
f. TABAINI
Ni
kusisitiza mambo kwa kutumia vikarushi. Baadhi ya semi zina dhana ya ukinzani
lakini kwa hakika hakuna ukinzani kimaana. K.m si salama si chochote hakuna
kilichotaka kinywani.
g. TASHBIHI
Yaliyopita
huja kama nguvu za sunami.(uk 45) Machupa hutafuna na kupuliza kama panya.
h. BALAGHA
Hayahitaji
majibu.
Anasema
nini?
Itakuwaje
sisi wawili ndio tuwe najibu?
6. MAEKO
Hadithi
inapoanza ni usiku wa manene ambapo Hamduni au Duni anaporejea kwake. Anatoka
ulevini kama ilivyokuwa desturi yake. Ni majira ya usiku wa manane. Anaimba wimbo wake wa kawaida ambao mwandishi
anaita “taarabu njia.” Kwani alizoea kuuimba akiwa njiani kuelekea kwake.
Jamila mkewe
Hamduni anapomsikia mumewe anamka ili kumsubiri. Mwanzoni mumewe anamka ili
kumsubiri. Mwanzoni mumewe anaonyesha furaha na bashasha kwa kupokelewa na
mkewe. Lakini anageuka na kuwa mjeuri mkewe anapojaribu kumsaidia kupanda ngazi
za kuingia kwao puia anampiga mkewe teke kwa kukawia kumpatia chakula.
Mwandishi
anasema ghasia na zogolaukorofi wa duni zilidi na kukosesha utulivu katika ndoa
yao. Majirani na hata jamaa zake jamila walipoona kipigo kimezidi walimshauri
ajiondoe kwenye ndoa hiyo. Hata kuna kifana kwa jina salim aliyoyapitia.
Alitaka Jamila amwasi duni halafu angetoroka naye.Alishindwa kuelewa Kwa
hakika. Salim alimpenda kwa dhati au alitaka kujinufaisha kutokana na hali yake
Jamila.
Kwa sababu
ya madhila aliyofanyiwa na mumewe Jamila
ya kawaida. Alirauka asubuhi na kutayarisha kiamsha kinywa cha kukata na shoka
ambacho alikiagizwa kwa fujo. Kenyoye Duni alimpumbaza mkewe kwa mapenzi yasiyo
ya kawaida. Alirauki asubuhi na kutayarisha
kiamsha kinywa cha kukata na shoka akakusanya nguo zote chafu na
kuziroweka ili azifue baadaye kasha akaenda kumwita mkewe. Alimuomba msamaha
mkewe kwa yale yote aliyomtendea kasha wakashebeha.
Baada ya
hapa maisha yakawa ni yay ohayo amani na mapenzi kwa muiezi miwili, kufarakana,
kuombana msamaha, amani na kadhalika.Hta Jamila mwenyewe alishindwa afanye
nini. Lakini kwa kiasi kikubwa aliridhishwa na ndoa yake licha ya matatizo
aliyoyapata humo.
DHAMIRA
Watu
huvimilia mapato wanayoyapata katika ndio hiyo k.m. jina, pesa, mapenzi na
kadhalika.
MAUDHUI
1. ULEVI
Unywaji
pombe kupindukia.
Hamduni
alilewa kupita kiasi.Mwandishi anataka kukashifu ulevi.
2. UVUMILIVU
Jamila
amevumilia mateso na majirani wanavumilia kero za hamduni.
3. DHULMA KATIKA NDOA
Hamdunio
anamwacha mkewe na kwenda kulevya.
Kumchapa
Jamila akiwa amelevya.
4. MAEKO
Namna
ambavyo mtu (Jamila) amewekwa.
Jamila
anavumilia dhulma za ndoa kwa kuwa anapewa pesa, mapenzi, anafanyiwa kazi.
WAHUSIKA
1.HAMDUNI
Ni mhusika
mkuu katika hadithi hii na ni mumewe Jamila.
SIFA
1. MLEVI
Analewa kila
siku
2. Mwenye fujo
Anampiga
mkewe.
3. Ni mkaidi
Alikanywa
kupiga makelele usiku lakini anazidisha.
4. Ni msumbufu
Aliimba
usiku watu wakiwa wamelala.
5. Ni msanii
Alipenda
kuimba.
6. Ni mwenye majuto
Hujitia
makosa ambayo alitenda akiwa amelala.
7. Ni msahaulifu
Anasahau kwa
haraka aliyomfanyia mkewe.
8. Ni mwenye mapenzi.
Anampenda
mkewe.
2. JAMILA
Mhusika mkuu
ni mkewe Hamduni.
SIFA
1. Mwanamke mwenye umri mdogo.
2. Ni mvumilivu. Anavumilia masaibu ya
ndoa.
3. Mwenye mapenzi.
4. Ni mjinga anaishi katika ndoa kwa
sababu ya maeko.
5. Ni msamehevu anamsamehe mumewe kwa
aliyamfanyia.
6. Ni mwenye kutamani kuishi maisha
mazuri.
7. Mwenye matumaini
8. Mwenye msimamo thabiti hakutaka
kutoka kwa mumewe ingawa alishauri afanye hivyo.
3. SALIM
Ni rafikiye
Hamduni.
SIFA
1. Ni mnafiki. Alimwahidi Jamila amuasi
duni ili angeweza kutoroka naye.
2. Ni mwenye mawaidha ya kupotosha.
Anamhimiza Jamila atoke kwa duni ili aepuke kuhapo.
3. Ni msaliti. Anamtaka Jamila ambaye ni
bibiye rafiki yako.
4.WANAKIJIJI
1. Wanapenda amani
2. Wanamshauri Jamila.
3.
Ni
wavumilivu.
4. SELA
Ni
mhusika mkuu anasomea shule ya Askofu Timotheo mwanawe mzee Buteli.
A) Ana utu na huruma. Hakuavya
mimba pia alipokutana na Masazu aliyejifanya
mgonjwa , alimsaidia.
B) Ni mkarimu. Anampeleka
Masazu kwenye kliniki.
C) Mwenye mapenzi ya
dhati. Anampenda Masazu kwa moyo mmoja
anampenda ata baada ya kumpa ua uzito.
MBINU ZA SANAA
Ø NYIMBO
Mwandishi
ametumia nyimbo kwa nia ya kuwasilisha ujumbe Fulani kuonyesha hulka ya
mhusika.
Wimbo wa
kwanza unaimbwa na Hamduni anapotoka ulevini kuonyesha kuwa hakujali
walivyosema wasebuleni.
Ø MAJAZI
Mwandishi
amewapa wahusika majina yaliyolingana na sifa au hulka zao.
Jina la duni
halisi lilikuwa Hamduni lakini watu walizoea kulifupisha na kuwa Duni ili
litamkike kwa urahisi. Jina hili lilimfanya adharauliwe na watu mtaani
sebuleni.
Salim
alikuwa rafikiya Duni ambaye aliyejitolea kuleta hali ya utulivu katika maisha
ya Jamila kwani alijiona salama na bora kuliko Hamduni.
MBINU ZA LUGHA.
I. KEJELI
Duni mtiribu
sababu alizoea kuwaamsha majirani zake kwa nyimbo za kilevi. Duni hakuwa
mtiribu, hii ni kejeli kwa sababu aliwaudhi wanakijiji kwa nyimbo zake.
2. METHALI
m.f.
tunaambiwa kuwa wenyeji wa Sebleni walitoa maneno ya kumlaani Duni akini
yalikuwa ni “ dua la kuku haimpati mwewe” yaani Duni, maanake hakubadilika wa
kushughulishwa na hayo.
3. MISEMO
“usiku
mkubwa” (uk 66) usiku sana. “ kusafiri kwa mapana na marefu” kusafiri sana. “
mjaliwa laana” mtu aliyelaaniwa.
5. BALAGHA
Mwisho wa
haya utakuwa lini ya Rabi? (uk 67) alijiuliza Jamila hakuwa nalo.
6. KINAYA
Walimwonea
Jamila huruma walisema kuwa huko nje kulikuwa wanaume waungwana na majina na
staha zao na ambao wangefanya lolote ili wampate Jamila.
7. UTOHOZI
Baadhi ya
maneno yametoholewa kutoka kizungu ili kuonyesha usasa na pia athari za kizungu
kwenye maisha ya wahusika.
k.m: stimu-
steam
Kozi- course
Bendeji- bandage
Hai- high
Dii – dear
8. TASHBIHI
Alimpiga mkewe kama ngoma ya kimanga popote
apatapo kuonyesha jinsi Duni alivyimpiga mkewe bila huruma.
9. TAKRIRI
Maneno na
semi au kauli zimarudiwa ili kutilia mkazo wazo Fulani k.m mtiribu.
No comments:
Post a Comment