KANDA LA USUFI
Hadithi
inaanza kwa kisengere mbele kwa kurejelea jambo au tukio lililotokea mwishoni
mwa hadithi selaha masazu walikuwa wameenda kumchukua motto wao waliyempata
wakiwa bado wanafunzi.
Vijana hawa
walikutana wakiwa shule ya upili Sela katika shule ya Askofu Timotheo naye Masaru
akiwa shule ya Lenga juu. Urafiki wao unakita mizizi na kupeleka sela kupata
mimba na kufukuzwa shuleni.
DHAMIRA
Mwandishi
anataka kuonyesha kuwa mzigo wa mwenzioi huwa mwepesi kwako ilhali ni mzito
kwake. Wavulana na wanaume watauona mzigo wa kuwa na mimba kama mwepesi lakini
kwa wasichana au wanawake mzito.
MAUDHUI
1. Mapenzi
Sela na
Chris ni wapenzi kwani mapenzi yalishamiri baina yao.
2. Urafiki
Palikuwa na
urafiki baina ya Sela na Chris na baadaye wakawa wapenzi.
3. Usaliti
Usaliti nni
kumtendea mtu jambo kinyume na imani yake kwako. Masazu alimsaliti Sela kwa
kutowajibika katika kuchukua jukumu la kumwitikia Sela kwani ni mimba yake.
4. Elimu
Chris na
Sela ni wanafunzi na wanacheza na elimu yao kwa kutotilia maanani shuleni.
5. Majuto
Babake Sela
anajuta kumpeleka Sela shule. Sela na Mavazu wanajuta.
6. Umaskini
Kwa
umaskini, Sela hangepata nguo za kuvalisha kadogo(mtoto) kwani alivalishwa
matambara.
7. Kazi
Chris
anapomaliza elimu yake, alienda kutafuta kazi.
8. Ujanja
Chris
anatumia ujanja na kumwambia Sela kuwa ni mgonjwa ili amwongeleshe Sela.
9. Ndoa
Sela na
Chris wanapanga kuishi pamoja.
10.Ushawishi
Sela
anamshawishi Chris wamwendee motto wake ili upweke uuondoke.
11.Ukatili
Babake Sela
anawafukuza mamake na Sela nyumbani.
12.Ushauri
Mwalimu mkuu
anawasihi wazazi wa Sela kumtafutia Sela shule.
Wazee wa
jamii wanamshauri babake Sela kumrudisha kwa
jamii zake.
13.Utu
Sela
hakuavya mimba.
Razina
halati ya Sela anamlisha kadogo.
Sela na
mamake walipokelewa na watu wa karibu.
14.Msamaha
Babake Sela
aliwarudisha mamake na Sela.
WAHUSIKA
1. Sela
2. Masazu
3. Kadogo
4. Rozina
5. Mzee Butali
6. Bi. Magret
7. Mama Sela
8. Sista
Ingawaje
aliweza kuendelea na masomo yake katika shule ya kutwa ya hapo karibu na kwao.
Baada ya kujifungua alikaa nyumbani kwa miezi mitatu akikitunza kitoto chake.
Baadaye alimwachia mamake na kurudi shuleni.
Baada ya
masomo yake Masazu, alihamia mjini Dafina kutafuta kibarua, na kupata cha
kuvuna mkonge upweke na akaonolea kuwa jambo la busara kama angekuwa na mwana wo,
kadogo ili amtoe apweke wakati Masazu akiwa kazini.
Sela na
mchumbaye waliamua kumwendea mwanao hadi kule kijijini alimokuwa akikaa na
halati ya Sela, walipanga safari yao usiku na ikatokea kuwa kulikuwa na mvua
iliyosababisha unyevu na utelezi. Walipokuwa njiani wakirudisha Sela na mtoto
mgongoni, aliteleza na kuanguka kwenye mto uliokuwa umefurika na kusombwa na
maji pamoja na mwanao kadogo.
Masazu
alipoona hivyo alijitosa majini ili kuwaokoa. Hadithi hii inapoishi hajabainika
kama Masazu aliweza kuwaokoa . Hadithi hii inapoisha hajabainikakama Masazu
aliweza kuwaokoa au labda pia alisombwa na maji. Hadithi inaisha kwa taharuki.
MBINU ZA KISANAA
Ø Mbinu rejeshi
Ø Taharuki
Ø Maswali ya balagha
Ø Taswira
Ø Sadfa
1. Mbinu rejeshi
Hadithi
inahusu kumwiba motto lakini mwandishi atarejesha nyumba vile walivyopatana.
2. Maswali ya Balagha
Haya ni
maswali ambayo hayahitaji majibu. K.m mama Sela aliuliza Masazu, “ huyu si
mtoto wetu sisi wawili?”
Bw. Butali
aliuliza,” mama gani anayemtazama mwana akigeuka afriti?”
3. Taswira
Hii ni picha
ijengewayo mawazoni. K.m. Masazu anachomeka kidole chake ardhini na kula kiapo
cha mapenzi yake kwa Sela.
Masazu
akiweka vidonge vya dawa kwa mdomo na kumeza kwa maji.
4. Taharuki
Mwandishi
anatueleza kuwa Masazu anapokula kiaop nakiwiliwili cha Sela kinalengezwa na
mengine yaliachiwa yalibaki katika himaya ya maumbile.
5. Sadfa
Sela na
Masazu walikutana bila kutafutana na baadaye kuoana.
Bw. Butali
hakutarajia mambo aliyokumbana nayo yafanyike kwake.
Christine
MBINU ZA KISANAA
1.Mbinu rejeshi.
-Hadithi inahusu mapenzi ya Sela na Masazu.
-Mwandishi anaturudisha nyuma mahali ambapo
Masazu na Sela walikutana.
2.Maswali ya balagha.
-Mamake Sela anamuuliza babake Sela kwani
Sela si msiba wao bali wa mamake tu.
-Masazu anauliza Sela kwa nini hakujikinga.
3.Taswira.
-Hii ni picha ya mawazoni.
-Hii inajitokeza ambapo Masazu anakichomeka
kidole chake ardhini akiwasilisha kiapo kwa Sela kuwa mapenzi yake ni ya dhati.
4.Taluki.
-Hali ya kutojua kilichotendeka hapo mbeleni.
-Ambalo Sela na mtotowe wanatumbukia majini.
-Wakati ambapo Masazu aliapa kiapo aliyeyusha
nafsi ya Sela na hatukwambiwa nini ilitendeka.
5.Sadfa.
-Haya ni mambo ambayo hayakutarajiwa
kutendeka.
-Sela na Masazu walioana hata baada ya Masazu
kumsaliti.
MBINU ZA LUGHA
1.TASHBIHI
Hulinganisha
kitu na kingine k.m;
·
Kiwiliwili
chake mithili ya mbwa anayekabiliana na chatu macho kwa macho.
·
Ulimwengu
wake ulivurugika, akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaendaarijoyo.
·
Nafasi
kama hiyo hutokea kwa nadra ya jua kupatwa na chui aliyelivizia windo lake na
sasa limetokea, akajiandaa.
2. Tashhisi
Sifa ya
kukipa kitu chenye hakina uhai( uhaishi)
·
Mambo
haya mawili yalielekeaa kuungana kuhujumu mkakati wao.
·
Matone
yalitua sehemu yao ya hujuma. Mwandishi arejelea pale ambapo Sela na Masazu walikuwa
wamejificha chini ya mwembe.
·
Mabaki
yalielekea kutapika wanafunzi wakikena kiume.
3.Semi.
·
….baridi
shadidi ya usiku(uk59)ina maana kuwa huo ulikuwa na baridi kali.
·
Alijaribu
kuvuta kumbukumbu(uk59)yaani alianza kukumbuka.
4.Methali.
·
Mimba
ile ya Masazu ilikuwa kanda la usufi.Methali hii inasema kuwa mzigo wa mwenzio
ni kanda la usufi.
·
Uchungu
wa mwana aujuaye mzazi.(uk63)
5.Istiara.
·
Nyumbani
mwa Butali kuligeuka kuwa jehanamu.
·
Mimba
ya Sela inalinganishwa na msiba.
·
Usiku
wa giza-kukosa matumaini.
SHAKA
YA MAMBO.
|
Alikuwa anaishi na mzee Mwinyi na familia yake katika mtaa wa Madaraka Estate
alipokuwa amekodisha nyumba.Mzee huyu alimchukua kama mwanawe.Pia alikuwa na
rafiki wa kiume aliyeitwa Kamata.Hatimaye anafika kazini,mkahawa uliokuwa
katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa J.K.I.A na kuanza kazi.Mkubwa wake Grace
hangeweza kushika zamu yake kwa sababu alikuwa na miadi yake lakini angemlipa
baadaye.Kamata alifanya ya kukagua ya wasafiri humo uwanjani.
Tunamuona mzungu mteja akiacha bunda la noti za dola ya
Kimarekani zaidi ya alfu moja.Esther
anachukua na kushindwa atazipeleka wapi.Kisha Kamata na Grace wanaingia na
kuanza kuchukua zile dola Kamata akidai
kuwa atampa mwenyewe pesa.Ajabu ni kuwa Kamata hakumwona yule mzungu
tena.Angemjuaje?Kisha Esther na Kamata
walikuwa wakisuhubiana.Esther akawaza kuwa Kamata hawezi mjua abiria huyo
kwani hakumweleza wasifu wake.
Maudhui.
Ni adhali ya
maisha ya mjini hasa kwa vijana watafutao kazi.
Kazi.
Tunamuona Esther akielekea Nairobi kutafuta kazi.
Unafiki.
Kamata anajifanya mwema na kuchukua zile pesa na hajui
anayempelekea.
Uaminifu
Esther anaaminika kwa kazi yake.
Elimu.
Esther amesoma na bado anataka kuendeleza masomo.
Shaka(kukosa
uhakika)
Esther anashaka kuwa Kamata atarudisha zile pesa.
6 .Usasa na
mabadiliko.
Zamani wanawake hawakuelimishwa lakini swala hili limeingia ambapo Kamata
anampisha Esther kiti kwenye gari.
7.Uajibikaji.
Esther aliwajibika kazini mwake.
8.Uvumilivu.
Esther anavumilia akidhani atabadilishwa zamu.
9.Usaliti.
Grace anamsaliti
Esther kwa kuwa na uhusiano na Kamata.
Wahusika.
1.Esther.
-Ni mhusika mkuu.
-Ametoka Machakos.
-Anafanya kazi ya hoteli J.K.I.A
-Anaishi kwa mzee mwinyi.
Sifa.
1.Mwajibikaji.
Aliajibika kwa kazi yake katika hoteli.
2.Mshamba.
Anadanganywa kwa rahisi sana.
3.Mvumilivu.
Alisubiri ili abadilishwe zamu.
4.Mwoga.
Hakutaka kuambia Kamata anampenda.
5.Mwenye shaka.
Alishaka kwa vile pesa zitamfikia yule mzungu.
6.Mwadilifu.
Hajiingizi katika mapenzi ya nje ya ndoa.
7.Mwenye
mapenzi ya dhati.
Anampenda Kamata.
8.Mwaminifu.
-Alipopata zile dola alimrejeshea mteja.
-Anashawishika kwa urahisi.
2.Kamata.
-Ni mfanyikazi katika uwanja wa J.K.I.A
-Ni rafikiye Grace.
-Anapenda starehe na anasa.
Sifa.
1.Ndumakuwili.
-Ana uhusiano na Grace na Esther.
2.Mlaghai.
Anamdanganya Esther.
3.Msaliti.
Anamsaliti Esther mapenzi yake.
4.Hana subira.
Aliona gari la Esther limekaa na kuingia kwa Grace.
3.Grace.
-Ni rafikiye Kamata.
-Ni mkubwa wa Esther kazini.
Sifa.
1.Mpenda anasa.
Anaenda vilabuni kisiri na Kamata.
2.Msaliti.
Anamsaliti Esther.
3.Mwenye tamaa.
Anatamani bunda lile na dola la mzungu.
4.Msiri.
Hakumweleza Esther
wanaenda na nani.
5.Mwongo.
Wana uhusiano na Kamata na kumdanganya ya Esther kuwa
hawana uhusiano na Kamata.
MBINU ZA LUGHA.
1.Maswali ya
balagha.
Kuna maswali ya kuchochea hisia na ambayo hayana
majibu.kwa mfano.
Esther anapokuwa kazini anawaza sana kumhusu
Kamata.Anajiuliza maswali ya balagha kama Kamata kweli anamjali naye huyu pia
anashughulika kutafuta pesa.
2.Utohozi.
Baadhi ya maneno ya kizungu yametamkwa kama ya
Kiswahili.km kompyuta-computer,disko-disco,blauzi-blouse.
3.Mbinu
rejeshi.
Inatumika katika (uk4) ambapo mwandishi anaturudisha
nyuma katika maisha ya babake Esther.
4.Tashhisi.
Hali ya kuvipa vitu visivyo hai sifa za vitu vyenye uhai.
NDOA YA SAMANI
Hadithi hii inasimuliwa
katika nafsi ya kwanza.Mwandishi amechukua nafasi ya mhusika mkuu,Abu na
kumtumia kusimulia.Hadithi inaanza kwa kisegere nyuma.Mbele kwa sababu
msimulizi anaanza kwa sehemu inayopaswa kuwa ndiyo ya mwisho wa hadithi.
Abu anaeleza kuhusu harusi
iliyokuwa ikifanyika kati yake na Amani.Mwanzoni Abu alitaka kumuoa Amali
lakini kwa kuwa alikuwa maskini wazazi wa amali wakakataa.Baadaye alipata kazi
ya uhamali Arabuni na kuweza kujiwekea akiba iliyomsaidia kuanzisha biashara ya
uchukuzi wa abiria na kutajirika sana.
Kwa kuwa hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na msichana
yeyote,marafiki zake walimshauri amrudie
Amali wake.Abu alirudi kwa akina Amani ili kumposa tena safari hii lakini
wazazi wa Amali hawakumkatalia posa yake hasa kama ilivyokuwa desturi
yao.Wazazi wa Amali walimshauri Amali
aagize kununuliwa zawadi tele na za bei ghali na Abu.
Ikawa pia harusi sharti
ifanyiwe nyumbani mwa Amali na tena iwe kukata na shoka.Siku ya arusi ilipofika
kila kitu kilikuwa shwari lakini Abu alikataa kushiriki katika awa hii na hivyo
basi arusi ikavunjiliwa bali.Abu alisihi kuwa Amali hakumpenda yeye bali
aliyapenda mali aliyonayo sababu ya Abu kufikiri hivi ni kuwa sababu Amali
alikuwa amemkataa alipokuwa maskini.Harusi iliyotarajiwa haikutendeka bali
iliwaacha watu vinywa wazi.
Dhamira.
Ndoa yapaswa kujengwa katika msingi wa mapenzi si
wa mali.Mwandishi anataka kutufundisha kuwa ndoa nzuri si ya pesa.
Maudhui.
1.Ndoa.
Msimulizi alimtaka Amali
amwoe lakini kulikuwa na katizi kwa upande wa mvulana kwa kuwa hakuwa na
pesa.Inatufunza usiolewe kwa sababu ya mali.Ndoa iwe ni maamuzi ya wenye
kuoana.
2.Umaskini.
Msimulizi alikuwa ametoka
kwenye familia ya kupigiwa mfano.Mwandishi anazingatia swala la umaskini lisiwe
zingitiki kwa mapenzi.
2.Tamaa.
Mamake Amali alikuwa na
tama ya kutajirika ndio maana alimkataa mwandishi mwanzoni.
4.Kisasi.
Msimulizi alilipiza kisasi
kwa kukataa kumwoa Amali kwa vile yeye alikahaliwa mwanzoni.
5.Usaliti.
Amali alisalitiwa na
msimulizi aliyemtoroka siku ya arusi.Mamake Amali alimsaliti mwandishi kwa
kumkataza mwanzoni aoe Amali.Pia alimsaliti Amali kwa kumkataza aolewe na
mwandishi.
6.Changamoto.
Mwandishi anapitia mambo
magumu .mfano;Umaskini,kukosa kazi na pia kukataliwa na mamake Amali.
7.Bidii.
Mwandishi alienda Arabuni na kujikaza na kuwa tajiri.
8.Utajiri.
Mamake Amali anataka
kutajirika.
Wahusika.
1.Mwandishi.
Ni mhusika wa kiume
anayopitia mambo magumu maishani.
Sifa.
1.Mchochole.
Kwao walikuwa maskini wa
kupigiwa mfano.
2.Mwenye bidii.
Alipopata uajiri Arubani,
alitia bidii na kutajirika na kuweza kujenga nyumba yake pamoja nay a wazazi
wake.
3.Msaliti.
Alimsaliti Amali kwa
kukosa kumuoa.
4.Mwenye kisasi.
Alikataa kumuoa Amali kwa
vile alikataliwa hapo zamani kumwoa na Mamake Amali kwa kuwa hakuna na pesa.
5.Mkarimu.
Aliitikia kununua vitu
ambavyo alivyopendekezwa kununulia familia yake Amali ili amuoe.Pia
aliwatafutia ndugu zake kazi huko Arabuni.
2.Amali.
Msichana aliyetakiwa
kuolewa na msimulizi.
Sifa.
1.Mtawa.
Anakaa kwao nyumbani na
kutojishughulisha kwenda kufanya mapenzi kiholela.
2.Mtiifu.
Anawatii wazazi wake na
pia dini yake.
3.Mrembo.
Wengi walimtaka kwa sababu
ya urembo mwandishi aliyesoma.
4.Mtamaduni.
Alifuata mambo ya
kitamaduni.
3.Wazazi wa Amali.
(i)Mamake.
Sifa.
1.Mwenye tamaa.
Anaitisha mahali ya
bintiye ili atajirike.
2.Mwenye ubinafsi.
Anajiitishia vitu vyake
pekee kama mahari ili Amali aolewe.
Mtindo wa lugha.
Ametumia misemo .kwa
mfano;
Kupata jiko-kuoa
Walalahai-tajiri
Walalahoi-maskini
Maskini hohehahe-umaskini
MIZIZI NA MATAWI
Hadithi hii inatusimulia
kisa cha mvulana mmoja kwa jina lake Sudi.Alilelewa na mama tajiri
aliyemsomesha hadi chuo kikuu na mwishowe akaajiriwa.Alizoea kuuliza kama
alikuwa na babake mzazi tangu utotoni akajulizwa kuwa babake mzazi ni Abdalla
lakini hajawahi muona.
Siku moja alimuuliza
mamake aliyetengeneza hadithi ya uongo kuwa Abdalla alimkimbia akiwa bado
hajamzaa Sudi.Jioni moja Sudi akitoka stareheni zake alikutana na mwanamke
mmoja aliyemwomba usaidizi.Alimpeleka
hadi kwao na kumwajiri kama yaya.Bibi huyu alimsimulia Bi.Mkubwa jinsi alivyomtupa mtoto kwenye pupa
la taka kwa kukosa uwezo wa kumlea.
Baadaye Bi.Mkubwa
alimweleza Sudi kuwa mamake mzazi ni yule mfanyikazi wake na kuomba
wasameheane.
Dhamira.
Hadithi hii inatufunza
kuwa hata mtu akipotelewa na waliokaribu naye ama wakose kumsaidia bado anaweza
kuendelea na kufaulu maishani.
Maudhui.
1.Mapenzi.
Sudi alipendwa na
wasichana wawili Radhia na Waridi.Wasichana wengine pia walimpenda Sudi kwa
utanashati wake.
2.Ukatili.
Bi.Kudura alifanya ukatili
kwa kumtupa mwanawe kwenye pipa la takataka.Alijua hili lilikuwa kama kuua
lakini hakujali.
3.Majuto.
Bi.Kudura anajuta kwa
kumtupa mwanawe na baadaye hakuweza kupata mtoto aliomba Mola amsamehe.
4.Uana haramu/malezi.
Sudi hakumjua babake jambo
lililomsumbua sana kimawazo.
Alimuomba mamake amwambie
ukweli lakini alimdanganya.
5.Elimu.
Licha ya kuwa
mwanaharamu,Sudi alisomeshwa na mamake hadi kiwango cha juu hadi akawa daktari.
6.Anasa.
Sudi alipokuwa ulaya
alihudhuria sherehe iliyokuwa ya kukata na shoka ambayo ilikuwa ni sikukuu ya
pasaka.Kulikuwa na muziki na wanawake wengi walitaka kucheza na Sudi.Pia
alimpeleka mpenziwe Radhia kustarehe huko.
WAHUSIKA.
1.Sudi Abdalla.
(a)Mtana shati.
Ni kijana aliyependa usafi
sana kwani tunamwona akijikwatua alipokuwa akijiandaa kwenda karamuni.
(b)Mkarimu.
Mara kwa mara alimpata
Bi.Kudura njiani na hakumpita .Alimpa msaada aliotaka.
(c)Mwenye heshima.
Aliwaheshimu mamake na
Bi.Kudura .Licha ya kuwa Bi.Kudura alikuwa maskini mwombaji,Sudi alimwita kwa
majina ya heshima.Pia hakuwahi kumtuma amletee chochote.
(d)Mwenye utu.
Kutokana na utu
wakealimsaidia Bi.Kudura.Alimwonea huruma alipompata njiani karibu na makaburi.
(e)Anapenda anasa.
Anapenda kuhudhuria
karamuni na sherehe na mpenziwe Radhia.
(f)Mwenye mapenzi ya dhati.
Alimpenda sana mamake na
Radhia mpenziwe na kufanya uchumba naye.
2.Bi Mkubwa.
Huyu ndiye aliyemwokoa
Sudi alipotupwa kwenye pipa la takataka na mamake mzazi.Alimlea kama mwanaye.
Sifa zake.
1.Ni mwongo.
Alimdanganya Sudi kuwa
yeye ndiye mamake mzazi na kuwa babake
alikuwa akiitwa Abdalla lakini alikufa na kumwachia mamake ulezi.
2.Ni mkarimu.
Bi.Kudura alipopelekwa
kwake alikubali kukaa naye na hata akampa vitu alivyoagizwa na Sudi.
3.Ni msiri.
Aliweza kuiweka siri juu
ya asili ya Sudi kwa muda mrefu tangu Sudi akiwa mtoto.
4.Mwenye mapenzi ya dhati.
Bi Mkubwa alimpenda Sudi
na kumlea kama mwanaye.
5.Msamehevu.
Alimsamehe Bi.Kudura naye
akasamehewa na Sudi.
3.Bi.Kudura.
Huyu ndiye aliyemzaa Sudi
nje ya ndoa na kumtupa kwenye pipa la takataka kwa sababu aliona aibu.
Sifa zake.
(a)Ni mkatili.
Alifanya ukatili kwa
kumtupa mtoto mchanga kwani hakujua kama angeokotwa na mtu au angeliwa na
mnyama.
(b)Ni mnyenyekevu.
Kwa sababu ya hali yake ya
umaskini alinyenyekea ili asaidiwe.
(c)Ni mcha mungu.
Alijua kuwa tendo la
kumtupa mwanawe ilikuwa dhambi kwa mungu.
MBINU ZA SANAA NA LUGHA.
1.Taharuki.
Sudi alikuwa na hamu ya
kumjua babake mzazi.Naye mamake alimweka na taharuki kwa muda mrefu.
2.Methali
-Mungu akikupa kilema
hukupa na mwendo.Sudi alitaka mamake amwambie ukweli ndipo ajue jinsi ya kuishi
na ukweli huo.
-……yaliyopita huwa
yamepita.Sudi alitaka kuyasahau maisha ya anasa aliyoishi alipokuwa ulaya.
-Kuvyaa kupona.Mwanamke
anapopata mtoto,mtoto huyo atakuja kumfaa baadaye akiwa mkubwa.
-Damu ni nzito kuliko
maji.Bi.Kudura aliongozwa na kudura hadi ilipo damu yake na kumpata mwanawe
Sudi.
3.Misemo.
-Kata tama-kosa matumaini.
-Tulia kama maji ya
mtungi-tulia sana.
-Piga gari moto-Gurumisha
gari.
-Walikuwa hawajijui
hawajitambui-hawajiwezi.
-Piga moyo konde-Amua
kufanya jambo.
4.Maswali ya balagha.
-Furaha yangu itoke wapi
tena?
-Kuna ukatili gani zaidi
ya huo?
5.Kuchanganya ndimi.
Kwa mfano:Handsome,Tea
breeze,Royal palm.
6.Uzungumzi nafsia.
Sudi alijisemea mwenyewe
anaposema.’Kumbe ni kweli
wanavyoniita’Sudi alisaini kimoyomoyo.
Gari unahaishwa
tunapoambiwa kuwa Sudi alipiga gari lake moto na taratibu likatambaa na kuanza
masafa kuelekea lilikokusudiwa.
8.Jazanda.
Kwa Sudi maneno haya
yalikuwa msumeno unaokeketa kwa maumivu makti.
9.Tashbihi.
…..lakini ulimi wangu
mzito kama nanga.
10.Mbinu rejeshi.
Sudi anaturejesha nyuma
huko ulaya alipokuwa akisomea na
kutuonyesha jinsi maisha yalivyokuwa.
11.Sadfa.
Kukutana kwa Sudi na Bi.
Kudura ilikuwa sadfa kwani hakutarajiwa.
12.Utohozi.
Hoteli-hotel
Bia-beer
Muziki-music
Benki-bank
Densi-dance
13.Nidaa.
Sudi alikuwa
akitabasamu-tabasamu ya fahari kwa uzuri wake.
Alifariki ghafla na
kuniacha na mimba yako,tena changa!
Ikawa kama mtu aliyefundua
tandu akafundika nge.
Naam,watu walikuwa
wawiliwawili…ndume na mke!
Alimrudi kila mmoja alikuwa na ulimwengu wake.
Inanikumbusha kauli ya
wahenga …kuvyaa kupona!
Aa vile nao na umetulia!
Hapo kabsa!