MKE WANGU
Hadithi hii inaanza wakati ambapo msemaji alikuwa anachaguliwa mke
atakayeoa na wazee wake lakini hakutaka hivyo yeye alimtaka motto mbichi ambaye
angemvumbika mpaka aive. Pia alimtaka mke ambaye alikuwa na sifa ambazo
angetaka mke wake awe nazo. Alimweka Aziza rohoni mwake kwani alikuwa kinyume
na wasichana ambao walikuwa wamesoma. Alikwa amesoma skuli akapata kuwa mjuaji
sana. Msemaji anasema kuwa alipomaliza masomo yake ya juu,mamake alianza
kumshawishi kuhusu mambo ya ndoa. Mama
alimtajia wasichana kadhaa lakini aliwakataa wote na kusema kwamba alimtaka Aziza aliamua
kumwoa.
Baada ya harusi
na sherehe walienda fungate yao ambapo msimulizi alipata kumsoma Aziza na apate kumsomesha. Katika harakati ya
kumsoma Aziza,msimulizi aliona kwamba Aziza hakuwa na mazungumzo pamoja naye
,pia aliona jinsi alivyokuwa akimtazama kwa unyarafu. Alipoulizwa kwa nini
alifanya hivyo,alisema kuwa alimsikitikia kwani alimwona kama gumegume tu wala
si mume wake kwa sababu hakuwa anafanya
kazi yoyote isipokuwa kutembea tembe.
Aziza aliteta
pia kwamba mumewe alikuwa na mikono laini kiasi cha kuwa angemguza mwanamke
hangehisi chochote. Aziza hakuwa anavalia viatu kila alipokwenda, na
alipoulizwa mbona havalii alisema kwamba hataki kutegemea ngozi za ng’ombe
aliyekufa .
Msimulizi anasema
kwamba humwamrisha mkewe atakavyo
kutamshinda. Pia anasema kuwa anaona fedheha kuu,kwanialio kisonoko ambaye hangeweza kutoka naye
mbele za watu alishangaa jinsi atakavyoishi naye mbele za watu. Alishangaa jinsi
atakavyoishi naye kwa sababu hata mambo madogo ambayo ni muhimu hatilii
maanani.
Aziza alikuwa
amenunuliwa brushi ya meno na dawa ya meno lakini hakuvitumia hata
kidogo.Aliamua kumuuliza asili yake.
Msimuluzi
alipomuuliza kwa nini hakutumia brushi Aziza alisema kwamba ana mswaki wake binafsi ambao ulikuwa umetengenezwa
na mnazi na ndani mlikuwemo unga uliokaa kati kati baina ya jivu na
masizi. Aziza alisema kuwa hatautia mswaki ule mdomoni ati kwa sababu na manyoya ya nguruwe. Pia alisema kuwa
wanaotumia brashi baada ya miezi matatu ama mitano huenda kumwona daktari wa
meno.
Siku hiyo, Seluwa
mtoto wa shangazi yake aliwatembelea. Wazee wa msimulizi walitaka amwoe Seluwa
lakini alimkataa kwa sababu zake. Seluwa na Aziza walikuwa wakitaniana ‘mke
mwenzangu’ na pengine ‘wifi yangu’. Wakiwa katika mazungumzo yao Aziza
alismskia Bazazi wa madafu akipita huko nje. Msimulizi alimpa Aziza shilingi
mbili akanunue hayo,kasha Aziza akamwita Bazazi huyo aende nyumbani mwao.
Bazazi huyo alipofika humo, Aziza akamwambia bwanake kwamba
nia ya kumwita huko nyumbani ilikuwa ili aone kuwa alitaka bwana kama huyo.
Hayo ni kwa sababu daima alikuwa
anafikiri kazi tu. Baada ya kumwambia hayo,Aziza alimwambia bwanake aampe
talaka yake.
2. Wahusika
Hadithi hii ya Mke Wangu ina
wahusika wafwatao;
Msimulizi
Aziza
Fedhele Salim
Salma
Seluwa
Wazazi wa msimuliza
Wahudumu wa msimulizi k.v Mapanya
MSIMULIZI
Msimulizi ni mhusika mkuu
katika hadithi. Alizaliwa katika familia ya kitajiri kama anavyotueleza katika
ukurasa wa 18.. Ni kijana wa kisasa na mumewe Aziza.
Ni mtamaduni kwa sababu
anautii utamaduni wa jadi unaompendelea mwanamume.
Yeye ni msomi aliyesoma hadi
viwango vya juu vya elimu.
Aidha, msimulizi anaweza kuelezwa
kama mzembe kwa sababu hataki kujihusisha na kazi za sulubu kama vile
kuangusha nazi, kuchoma na kuuza mihogo pamoja na kazi nyinginezo. Anashangazwa
na uamuzi wa mkewe wa kutotaka kufuliwa nguo wala kuooshewa vyombo.
Ingawa tumemtaja kama mtamaduni,
Msimulizi anaweza kueleweka kama mwanausasa kwa sababu anampendekezea
mkewe kutenda mambo ya kileo kama vile kuvaa viatu na kupiga mswaki. Kwa sababu
hii, anadhihirisha tabia ya mtu asiye na msimamo dhabiti. Ukosefu huu wa
msimamo unamfanya ashindwe kujiamulia mambo muhimu maishani kama vile; mke wa
kuoa, kazi ya kufanya na namna ya kuiongoza familia yake changa. Kwa
maneno mengine, msimulizi ni mhusika aliyekengeuka na
asiyejifahamu.
Isitoshe, msimulizi ni mvumilivu na
mwenye subira kwa vile si mwepesi wa kutibukwa na hisia
tunadhihirishiwa kuwa anamvumilia Aziza kama mkewe licha ya fedheha anayoipata
mbele ya wageni wao wenye ustaarabu wa kimjini. Licha ya Aziza kumdharau,
kumwita gumegume na kumsuta kwa kutofanya kazi maishani, msimulizi haonyeshi
kuudhishwa na mkewe.
Badala yake, msimulizi anamkubali na
kumvumilia mkewe akitaraji kuwa siku moja atazinduka na kuukumbatia usasa na
ustaarabu. Aziza anafikia kiasi cha kumwita bazazi wa madafu kasrini mwao,
kumsifu bazazi wa madafu mbele ya mumewe na hata kumuomba mumewe talaka.
Msimulizi haonyeshi kukasirishwa na maudhi haya yote.
Ni mwenye taasubi ya kiume; hulka
hii inadhihirishwa pale ambapo anatarajia kumpata mke ambaye hakwenda
skuli. Nia yake ni kumpata mke ambaye hatakuwa katika ngazi moja ya kielimu
naye. Tunaweza kuhitimisha kuwa msimulizi hataki mwanamke mwenye ung’amuzi wa
usawa wa kijinsia na haki za wanawake. Kwa mujibu wake, matatizo ya ndoa
hutokana na midomo na ujuaji wa wanawake.
Aidha, anapanga kumvinya mkewe na
kumfunza mambo ya kisasa ya uanagenzi. Anammithilisha mkewe na tunda
linalohitaji kuvinywa. Anaonyesha dharau kwa wanawake kwa sababu
anawalinganisha na watoto wadogo ambao hawaachi kisebusebu (uk. 21)
Umuhimu wa msimulizi
Msimulizi ni mhusika mkuu katika
hadithi hii. Anaakilisha kizazi kilichochanganyikiwa. Kizazi kilichojipata
katika nja panda, yaani katikati ya ukale na usasa.
Mbali na kuchanganyikiwa, msimulizi
anaakilisha matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii ya kisasa kama vile mfumo
mbaya wa elimu inayolenga ajira, ukosefu wa ajira, ujuma na uzembe, matatizo ya
ndoa na kadhalika.
Msimulizi ni kielelezo cha jamii
ambayo inashindwa kuyaelewa mazingira yake. Anashindwa kuuelewa utamaduni wake,
mahitaji yake majukumu yake, na hata hamwelewi mkewe.
Waama, ni kupitia kwa mahusiano ya
Msimulizi na mkewe ndipo tunabaini kuwa elimu na hekima ni mambo mawili
tofauti.
AZIZA
Ni mhusika mwingine ambaye anaweza
kuutajwa kama mhusika mkuu. Ni mkewe msimulizi. Tofauti na msimulizi,
Aziza alizaliwa na kukuzwa shamba.
Aziza ana sifa zifwatazo;
Kwanza, Aziza ni mdadisi wa mambo.
Anamchuja msimulizi na kuugundua udhaifu wake. Ni kutokana na udadisi huu ndipo
anagundua kuwa yeye na msimulizi wako na mawazo yaliyobaidika.
Anaumaizi ulelemama wa mumewe wa
kutofanya kazi na tabia ya kutegemea wazazi wake. Anadadisi na kugudua viungo
vya dawa ya meno; tumbawe, sabuni na arki za peremende kali. Pia, anagundua
kuwa mswaki si lolote si chochote bali nywele za nguruwe.
Aziza anaweza kuelezwa kama mhafidhina,
anayapinga madai ya msimulizi kwamba riziki ya kazi imekosekana. Yeye
anashikilia kuwa mtu hawezi akakosa kazi ulimwenguni, kazi anazozitaj ni kazi
za jadi kama vile kuangusha nazi, kuchoma na kuuza mhogo na hata kuchunga
punda. Uhafidhina wa Aziza unazidi kujiidhihirisha pale anapokataa katakata
kuvaa viatu huku akishikilia kukanyaga chini kote aendako. Anawadharau wanaume
wa kimjini enye usasa na mwishowe anajiafadhalisha kuolewa na mwanamume wa
shamba.
Mwenye dharau; kila mara, Aziza anamchuja mumewe kwa dharau. Anavidharau
viatu, mikono ya mumewe, mswaki na dawa ya meno ya kisasa. Kitendo cha kumsifia
bazazi wa madafu mbele ya msimulizi pia ni ishara ya dharau.
Sifa nyingine ya aziza ni kuwa yeye
ni mwenye hekima, majibizano yake na mumewe yanadhihirisha hekima tele.
Anashangaa ni kwa nini walishwe na wazazi wa msimulizi. Anaumaizi udhaifu uio
kwenye dawa ya kisasa ya meno, anashangaa ni kwa nini wale waliotumia dawa ya
meno waliyang’oa meno yao kila wakati. Hekima hii inamfanya msimulizi kukiri
kuwa mkewe ni mtu asiyeweza kupatwa kiotoni.
Mwenye msimamo thabiti; Aziza anadhihirisha kuwa na msimamo thabiti kwa mambo
anayoyaamini. Anakataa kushawishiwa kuukumbatia usasa. Anashikilia na kuyaishi
maisha ya jadi hata kama kila mtu aliye karibu naye ameukubali usasa.
Anapojibizana na mumewe, Aziza
anajitokeza kama mhusika jasiri. Anakataa kuwekwa chini na mumewe. Hali
ya kutopata masomo ya kisasa haimnyimi uasiri wa kuaimama kidete na kuyatoa
mawazo yake. Kutokana na ujasiri wake, anamkabili mumewe na kuzishutumu tabia
zake bila hofu wala woga. Hatimaye, anamjulisha msimulizi kimasomaso kuwa
angetaka apewe talaka yake.
Umuhimu wa Aziza
Aziza amechorwa kama mhusika bapa
sugu. Anao msimamo sugu kuhusu utamaduni wa jadi na hakubali kuubadili
msimamo huu.
Anawakilisha watu wanaoshikilia msimamo
thabiti wa kuutetea ujadi. Aziza anaweza kutazamwa kama mdomo wa
mwandishi kwa sababu mwandishi amempa hekima nzito na amewezeshwa kumpiku
msimulizi katika migogoro yao mbalimbali.
Aidha, aziza ametumiwa na mwandishi kuutetea
utamaduni wa waafrika dhidi ya athari za kigeni kama vile elimu na mavazi.
Aziza ametumiwa kupitisha ujumbe
kuwa furaha na utu wa mtu si elimu wala utajiri wala ajira, bali maadili mema,
bidii, heshima na mapenzi ya dhati.
Kupitia kwa Aziza, tunajuzwa kuwa mwanamke
wa kiafrika amejikomboa kimawazo na anaweza kujifanyia maamuzi tofauti na
adhaniwavyo na wanaume wenye taasubi za kiume kama msimulizi.
Maswali
1. Jadili uhusika (hulka na umuhimu) wa msimulizi na wa Aziza
2. ‘Msimulizi na mkewe hawapatani kwa lolote’, jadili kauli hii
ukirejelea hadithi fupi ya Mke Wangu.
FEDHELE SALIM, SALMA NA SELUWA wanaweza kuelezwa kama wasichana wa kisasa;
msimulizi anawataja kama wasichana waliojaa utamaduni wa kisasa.
Fedhele anaelezwa na msimulizi kama msichana msomi. Ingawa
hivyo, tabia yake ya kuvalia kanzu fupi na kuandamana na wanaume hazimpendezi
msimulizi.
Salma anadhihirika kama msichana mwenye kujipodoa na
marangi ya mashavu na midomo.
Msimulizi anatueleza kuwa Seluwa
ana ‘kidomo’ yaani, ni mtu wa kuongea maneno mengi. Isitoshe, katika uk.
wa 24, anamtaja Seluwa kama msichana mwenye kujipodoa na
kupendeza.anamtaja kama mwingi wa bashasha, mizaha na furaha.
Umuhimu wa Fedhele, Salma na Seluwa
Hawa watatu ni wahusika wasaidizi.
Wanatusaidia kumwelewa msimulizi kwa
sababu wanatusaidia kujua ni mambo gani yasiyompendeza msimulizi.
Aidha, sifa zao zinakinzana na za
Aziza hivyo basi wanatusaidia kujua hulka za Aziza.
WAZAZI WA MSIMULIZI ni wakwasi kwa sababu msimulizi anatueleza kuwa yeye
alizaliwa katika familia ya kitajiri.
Wao ni wahifadhina kwa sababu
wanamlea mtoto wao kwa kuongozwa na tamaduni za jadi za kiafrika na hata
wanamchagulia mke kwa mujibu wa kaida za jadi za kiafrika. Msimulizi anatueleza
kuwa, …wazee wangu, juu ya utajiri wao, hawakupenda kubadili mila zetu… (uk.
18)
Mamake msimulizi anadhihirisha hekima
anapomwongoza msimulizikumchagua na kumwoa Aziza. Anapendekeza wasichana ambao
anajua msimulizi hatakubali kuwaoa.
Umuhimu wa wazazi wa msimulizi
Wazazi wa msimulizi ni wawakilishi
wa utamaduni wa jadi.
Maswali
1. Jadili uhusika wa msimulizi na Aziza
2. Je, Seluwa, Salma na Fedhele Salim wana umuhimu gani katika
hadithi
3. Unadhani ni kwa nini mwandishi akatumia anwani ya mke wangu
4. Ni vipengele vipi vya utamaduni wa jadi anavyovipendelea
mwandishi.
3.
DHAMIRA
Yaelekea kuwa mwandishi ana nia ya
kutubainishia kuwa Elimu ya jadi ni bora kuliko mafunzo ya kisasa ya shuleni na
vyuoni; hili linabainika tunapoona Aziza akipewa sifa ya kuwa mpevu wa hekima
nzuri na mwandishi.
Msimamo wa mwandishi ni
kuwa watu wa shamba waolewe na wenzao wa shamba na wale wa mjini waolewe na
wale wa mjini. Msimamo huu umetokana na yale anayoyaona katika jamii; migogoro
katika ndoa, ubaidi wa kifikra utabaka na mitazamo ya maisha inayokinzana.
Yamkini wimbi la kisasa ambalo
limeiacha jamii ya kisasa katika njia panda limemchochea mwandishi kuiandika
hadithi hii ili awakumbushe watu kurejelea kaida zao za jadi.
4.
MAUDHUI
Mafunzo yafwatayo yanajitokeza katika
hadithi ya Mke Wangu.
·
Utamaduni
·
Usasa na mabadiliko ya kijamii
·
Elimu
·
Utabaka, utengano na mitafaruku
·
Ndoa
·
Taasubi ya kiume na matatizo
yanayowakumba wanawake
·
Ukengeushi
1.
Utamaduni
Mohammed Said Abdulla anadhihirisha
utamaduni wa aina mbili.
Kuna utamaduni asilia wa Afrika
unaoendelezwa na Aziza na bazazi wa madafu. Aziza anaelezwa kama mwenyeji wa
shamba. Aidha anatetea na kudumisha mila za kiafrika kama vile bidii kazini.
Anashikilia kuyaishi maisha ya shamba kama vile kutovaa viatu.
Anapuuzilia mbali matumizi ya dawa
mswaki na dawa ya meno. Anakataa kuathiriwa na utamaduni wa kisasa.
Utamaduni wa kisasa unaendelezwa
nawahusika kama msimulizi, Seluwa, Fedhele na Salma.
Fedhele, Salma na Seluwa wanajipodoa
kwa vipodozi na rangi za kisasa.
Msimulizi anatetea uvaaji wa viatu,
matumizi ya mswaki wa kisasa na dawa ya kisasa ya meno.
Aidha, msimulizi ni mwanausasa
aliyeipata elimu ya kisasa, anaishi kwenye nyumba ya kisasa, anatumia mavazi ya
kisasa na vipodozi vya kisasa kama vile kitana.
Selume na msimulizi wanaamkuana kwa
kuingiana maungoni; mtindo ambao ni wa kisasa.
2.
Elimu
Elimu ni mfumo wa mafunzo
yanayopatikana shuleni, vyuoni au maishani.
Maudhui ya elimu yameendelezwa
kuwili kwenye hadithi ya Mke Wangu.
Kwanza ni yale mafunzo yapatikanayo
katika maisha.
Aidha, ipo elimu nyingine
inayopatikana vyuoni.
Japo Aziza ni msichana wa shamba,
anadhihirisha ukomavu wa hekima. Hii ni ishara tosha kuwa amebobea katikaa
mafunzo ya maisha kuhusu maswala ya kazi, ndoa, mahitaji ya jamii na matarajio
ya jamii kuhusu wajibu wa mume na mke ndoani.
Msimulizi na Fedhele ni wahusika
waliopokea mafunzo ya vyuoni. Wanatajwa kama wahusika waliopokea elimu ya hadi
viwango vya juu.
Hata hivyo, elimu hii iliyopokewa na
msimulizi inadhihirika kuwa duni kwa sababu haijamwezesha msimulizi
kujitegemea. Ni elimu yenye lengo la kupata kazi na wala hailengi kumsaidia mtu
kujimudu katika mazingira yake.
Aidha elimu hii inashindwa kumuhami
msimulizi na mbinu mwafaka za kuyakabili matatizo ya ndoa. Anashindwa
kuidhibiti ndoa yake na Aziza.
Kwa hivyo basi tunaweza kudadavua
kuwa mwandishi anaipendelea elimu ya jadi inayompa mtu mafunzo ya maisha dhidi
ya ile elimu ya kisasa inayopatikana shuleni na vyuoni.
3.
Utabaka na Utengano
Utabaka ni mfumo wa kijamii
unaowagawa watu kwenye makundi kutegemea uwezo wao wa kiuchumi au kijamii.
Kwa upande wake, utengano ni hali ya
watu kuwa mbali na wengine. Umbali hiu waweza kuwa wa kiuchumi, kijamii,
kijinsia, kimsimamo, kifikra au kimawazo.
Kwenye hadithi ya Mke Wangu, utabaka
unajitokeza pale tunapodhihirishiwa utajiri wa wavyele wa msimulizi na wakati
uo huo tunadhihirishiwa ufukara wa wahusika wengine kama bazazi wa madafu.
Maisha ya bazazi wa madafu nay a msimulizi yanatupa taswra kamili ya utabaka wa
kijamii.
Utengano wa kifikra pia unajitokeza
kati ya msimulizi na mkewe. Wawili hawa wanaakilisha misimamo pinzani kati ya
fikra za jadi na zile za kisasa.
4.
Ndoa
Ndoa ni makubaliano rasmi kati ya
mume na mke ya kuishi pamoja.
Ndoa zinazotajwa hadithini ni zile
za wazazi.
Ndoa zilizotajwa hadithini ni mbili.
Kwanza, ipo ndoa kati ya msimulizi na Aziza. Ya pili ni ndoa kati ya wazazi wa
msimulizi.
Ndoa kati ya msimulizi na Aziza
inakumbwa na matatizo si haba. Matatizo haya yanachimbuka kutokana na ubaidi wa
malezi ya wachumba hawa. Huku msimulizi umuhimu wa vyombo na mienendo ya
kisasa, Aziza anasisitiza kuwa mila, desturi na vyombo vya jadi ni lazima
vitekelezwe. Ndoa hii inaishia kwa Aziza kumwomba mumewe talaka.
Mwishoni mwa hadithi tunaashiriwa
ndoa mpya kati ya aziza na bazazi wa madafu.
Hatuelezwi sana kuhusu ndoa kati ya
wazazi wa msimulizi. Hata hivyo ndoa hii inaweza kuelezwa kama ndoa
inayoongozwa na kaida za jadi. Hii ni kwa sababu wanamuongoza msimulizi kumuoa
mke anayefwata kaida za jadi.
5. Taasubi ya kiume na matatizo yanayowakumba wanawake
Taasubi ya kiume ni mfumo wa kijamii
ambamo mwanamume hupewa nafasi ya juu kumliko mwanamume. Kwenye mfumo kama huu,
mwanamume hukumbwa na matatizo si haba.
Jamii ya mke wangu inaweza kuelezwa
kama inayoongozwa na mfumo huu.
Msimulizi anabainisha taasubi ya
kiume pale ambapo anawalaumu wanawake kwa matatizo yote yanayokumba ndoa.
Anapomwona Fedhele na wanaume, anamlaumu fedhele pekee yake na kuwapuuzilia
mbali wale wanaume.
Isitoshe, msimulizi anawadharau
wanawake na kuwalinganisha na watoto.
Aidha, msimulizi anamlinganisha
mkewe na tunda linalostahili kuvimbikwa ili live.
Hata hivyo, japo Aziza ni mwanamke
wa shamba, anajitokeza kama mwanamke aliyejikomboa kimawazo na mwenye hekima
tele.
6. Ukengeushi
Ukengeushi ni hali ya mtu kwenda
kando na uhalisia wa kijamii. Msimulizi, Fedhele Salma na Seluwa ni baadhi ya
wahusika ambao wamekengeuka. Maisha yao hayaingiliani na uhalisia wa mazingira
yao.
Japo, fedhele na salma wanajipaka
marangi kwa azma ya kuonyesha kuwa wamezinduka, tabia hii inawaudhi wanajamii
akiwemo msimulizi. Aidha, tabia ya Fedhele ya kutembea usiku na wanaume
inamuharibia sifa mbele ya msimulizi.
Msimulizi naye ni mhusika mwingine
aliyekengeuka, licha ya kuwa yeye ni msomi aliyefikia kileleta. Anapigwa chenga
na hekima ya msichana wa shamba. Aziza anamdhihirishia kuwa elimu yake
haikumfaa kwa lolote bali imechangia kumfumba macho ili asiung’amue uhalisia wa
kijamii.
Maswali
Eleza namna maudhui yafwatayo
yalivyoendelezwa kwenye hadithi ya Mke Wangu;
i)
Ndoa
ii)
Utabaka
iii)
Elimu
iv)
Ukengeushi
5. MATUMIZI YA LUGHA
Zifwatazo ni baadhi ya mbinu za
kisanaa na mbinu za lugha zilizotumiwa kwenye hadithi.
MBINU ZA KISANAA ni mbinu zote zinabuniwa na kutumiwa na msanii kuupitisha
ujumbe wake. Hizi ni pamoja na usimulizi, taswira, virejeshi nyuma, maswali
balagha, sadfa, chuku, kinaya, hadithi ndani ya hadithi.
MBINU ZA LUGHA pia huitwa tamathali za usemi. Ni matumizi ya vipengele vya
lugha vya kimapokeo kama vile methali, nahau, vitendawili, tanakali za sauti,
istiari na tashbihi.
1. Usimulizi
uliotumiwa kwenye hadithi ni wa nafsi ya kwanza.
Msimulizi
ni mmoja wa wahusika.
Anatusimulia
alivyozaliwa na wakwasi, akasoma hadi viwango vya juu na akachaguliwa mke wa
shamba na wazazi wake.
Anaendelea
kutusimulia kadhia zinazoikumba aila yake na migogoro inayoibuka kati yake na
mkewe.
2. Taswira mbalimbali
zinajitokeza kwenye hadithi ya Mke Wangu. Taswira ni picha zinazochoreka
mawazoni tunapozisoma kazi za fasihi. Pia huitwa jazanda.
Kutokana
na maelezo ya msimulizi, tunapata picha kamili ya Salma, Fedhele na Seluwa.
Fedhele na Salma wanachoreka mawazoni mwetu kama wasichana waliojirema na
kujipodoa kwa mapambo ya kisasa. Katika ukurasa wa 18, Fedhele anaelezwa kama
msichana aliiyevalia kanzu fupi na Salma kama mwenye kujipaka marangi.
Mbali na
kuwa mwenye kidomo, Seluwa anachorwa kama msichana mwenye kujipodoa, msichana
mcheshi na mwingi wa usasa.
Swali:
Eleza
picha inayokujia mawazoni;
Kumhusu
msimulizi, Aziza na bazazi wa madafu.
Kuhusu
mikono ya msimulizi na nyayo za Aziza.
3. Hadithi inaanza kwa kirejeshi nyuma. Tunarejeshwa
hadi enzi ambazo msimulizi alichaguliwa mke na ninaye. Kirejeshi nyuma hiki ni
muhimu katika kuielewa hadithi hii maana kinatupa usuli wa hadithi. Kirejeshi
nyuma hiki kinatufafanulia maswala ambayo ni msingi wa migogoro inayoibuka
hadithini. Matatizo yanayoikumba familia ya msimulizi yanatokana na vigezo
vibovu vilivyotumiwa katika kumchagulia msimulizi mke.
4. Maswali balagha:
… si lazima kwa hivyo, Aziza awe
mwepesi, msikivu, mwelekevu? (uk 18) msimulizi anatumia swali hili kueleza kuwa
maadam Aziza kakulia shamba, ni lazima hana jambo. Kwenye ukurasa wa 19, Aziza
anatumia maswali balagha kumbeza msimulizi, anauliza;
Mimi nilikuwa nikitazamia nitaolewa
na nani katika dunia hii? ...nitapata mume au gumegune tu kama wewe?
...basi wewe ndiye mume wa kunioa miye, we? …huoni wewe wala hupimi?
Katika mazungumzo yake na msimulizi,
Aziza anadhihirisha utumizi wa maswali balagha, taja na ufafanue umuhimu wa maswali
balagha katika maongezi ya msimulizi. (katika kulijibu swali hili, mwanafunzi
atafute na kutaja mifano zaidi ya maswali balagha kwenye hadithi)
5. Sadfa ni mbinu
ya kisanaa ambapo mambo mawili yanatokea kwa pamoja bila kupangwa. Inasadifu
kuwa siku ambayo Seluwa alimgeni msimulizi na kumwamkua kwa kumwingia maungoni,
bazazi wa madafu anapita akinadi madafu, hapo hapo Aziz anamwita ukumbini,
anaomba talaka kutoka kwa msimulizi na kumtaja bazazi wa madafu kama mume wake.
6. Chuku: ni mbinu
ya kisanii inayoeleza jambo kwa namna iliyotiwa chumvi. Katika kuisifia nyayo
za miguu yake, Aziza anadai kuwa miguu yake haidungiki kwa miiba. Kwamba hata
ukiushindilia mwiba kwenye nyayo zake, mwiba utavunjika!
7. Kinaya: ni kinaya
kuwa msimulizi anayepanga kumchanua Aziza anachanuliwa na Aziza.
8. Hadithi ndani ya hadithi: kwenye
hadithi ya Mke Wangu, msimulizi anaiwazia hadithi ya Nunez ambaye
alikuwa chongo na akafikiria kuwa angekuwa mfalme wa vipofu. Hadithi hii
inatusaidia kuelewa ung’amuzi wa msimulizi kuwa utamaduni wake na ule wa aziza
haungeingiana.
9. Methali
10. Nahau
na misemo iliyotumiwa hadithini ni pamoja na;
Elekeza rohoni (uk. 18)
inayomaanisha kumpenda mtu.
Weka kando inayomaanisha kupuuza
Mtoto mbichi ni msemo wenye maana ya
motto mchanga
Tia mguu mjini: pata kufika mjini
Kumvinya mwari: kumwelekeza mtu kwa
njia unayotaka wewe
Madarasa: mafunzo
Toa macho: kodoa macho
Zawadi za vicheko: kuchekeshwa
Kumtoa kinyanyaa: kumzindua mtu na
kumtoa ushamba
11. Tanakali
za sauti: aliondoka nyatunyatu
12. Istiara/
istiari
13. Tashbihi:
… kama mtoto anavyonyonya:
…wanawake ni kama watoto wadogo: hii
ni kauli ya msimulizi inayotubainishia mtazamo wa msimulizi kuwahusu wanawake.
…ngozi imekacha utafikiri msasa:
msimulizi anatumia tashbihi hii kuueleza mkono wa Aziza.
good work
ReplyDelete