Pages

Mwongozo wa Damu Nyeusi Part 4



KANDA LA USUFI

Hadithi inaanza kwa kisengere mbele kwa kurejelea jambo au tukio lililotokea mwishoni mwa hadithi selaha masazu walikuwa wameenda kumchukua motto wao waliyempata wakiwa bado wanafunzi.
Vijana hawa walikutana wakiwa shule ya upili Sela katika shule ya Askofu Timotheo naye Masaru akiwa shule ya Lenga juu. Urafiki wao unakita mizizi na kupeleka sela kupata mimba na kufukuzwa shuleni.

DHAMIRA

Mwandishi anataka kuonyesha kuwa mzigo wa mwenzioi huwa mwepesi kwako ilhali ni mzito kwake. Wavulana na wanaume watauona mzigo wa kuwa na mimba kama mwepesi lakini kwa wasichana au wanawake mzito.

 

 

MAUDHUI

1.     Mapenzi

Sela na Chris ni wapenzi kwani mapenzi yalishamiri baina yao.

2.     Urafiki

Palikuwa na urafiki baina ya Sela na Chris na baadaye wakawa wapenzi.

3.     Usaliti

Usaliti nni kumtendea mtu jambo kinyume na imani yake kwako. Masazu alimsaliti Sela kwa kutowajibika katika kuchukua jukumu la kumwitikia Sela kwani ni mimba yake.

4.     Elimu

Chris na Sela ni wanafunzi na wanacheza na elimu yao kwa kutotilia maanani shuleni.

5.     Majuto

Babake Sela anajuta kumpeleka Sela shule. Sela na Mavazu wanajuta.

6.     Umaskini

Kwa umaskini, Sela hangepata nguo za kuvalisha kadogo(mtoto) kwani alivalishwa matambara.

7.     Kazi

Chris anapomaliza elimu yake, alienda kutafuta kazi.

8.     Ujanja

Chris anatumia ujanja na kumwambia Sela kuwa ni mgonjwa ili amwongeleshe Sela.

9.     Ndoa

Sela na Chris wanapanga kuishi pamoja.

10.Ushawishi

Sela anamshawishi Chris wamwendee motto wake ili upweke uuondoke.

11.Ukatili

Babake Sela anawafukuza mamake na Sela nyumbani.

12.Ushauri

Mwalimu mkuu anawasihi wazazi wa Sela kumtafutia Sela shule.
Wazee wa jamii wanamshauri babake Sela kumrudisha kwa  jamii zake.

13.Utu

Sela hakuavya mimba.
Razina halati ya Sela anamlisha kadogo.
Sela na mamake walipokelewa na watu wa karibu.

14.Msamaha

Babake Sela aliwarudisha mamake na Sela.

 

 

WAHUSIKA


1.     Sela
2.     Masazu
3.     Kadogo
4.     Rozina
5.     Mzee Butali
6.     Bi. Magret
7.     Mama Sela
8.     Sista
Ingawaje aliweza kuendelea na masomo yake katika shule ya kutwa ya hapo karibu na kwao. Baada ya kujifungua alikaa nyumbani kwa miezi mitatu akikitunza kitoto chake. Baadaye alimwachia mamake na kurudi shuleni.
Baada ya masomo yake Masazu, alihamia mjini Dafina kutafuta kibarua, na kupata cha kuvuna mkonge upweke na akaonolea kuwa jambo la busara kama angekuwa na mwana wo, kadogo ili amtoe apweke wakati Masazu akiwa kazini.
Sela na mchumbaye waliamua kumwendea mwanao hadi kule kijijini alimokuwa akikaa na halati ya Sela, walipanga safari yao usiku na ikatokea kuwa kulikuwa na mvua iliyosababisha unyevu na utelezi. Walipokuwa njiani wakirudisha Sela na mtoto mgongoni, aliteleza na kuanguka kwenye mto uliokuwa umefurika na kusombwa na maji pamoja na mwanao kadogo.
Masazu alipoona hivyo alijitosa majini ili kuwaokoa. Hadithi hii inapoishi hajabainika kama Masazu aliweza kuwaokoa . Hadithi hii inapoisha hajabainikakama Masazu aliweza kuwaokoa au labda pia alisombwa na maji. Hadithi inaisha kwa taharuki.

 

 

MBINU ZA KISANAA

Ø Mbinu rejeshi
Ø Taharuki
Ø Maswali ya balagha
Ø Taswira
Ø Sadfa

1.    Mbinu rejeshi

Hadithi inahusu kumwiba motto lakini mwandishi atarejesha nyumba vile walivyopatana.

2.    Maswali ya Balagha

Haya ni maswali ambayo hayahitaji majibu. K.m mama Sela aliuliza Masazu, “ huyu si mtoto wetu sisi wawili?”
Bw. Butali aliuliza,” mama gani anayemtazama mwana akigeuka afriti?”

3.    Taswira

Hii ni picha ijengewayo mawazoni. K.m. Masazu anachomeka kidole chake ardhini na kula kiapo cha mapenzi yake kwa Sela.
Masazu akiweka vidonge vya dawa kwa mdomo na kumeza kwa maji.

4.    Taharuki

Mwandishi anatueleza kuwa Masazu anapokula kiaop nakiwiliwili cha Sela kinalengezwa na mengine yaliachiwa yalibaki katika himaya ya maumbile.

5.    Sadfa

Sela na Masazu walikutana bila kutafutana na baadaye kuoana.
Bw. Butali hakutarajia mambo aliyokumbana nayo yafanyike kwake.

 

Christine

MBINU ZA KISANAA

1.Mbinu rejeshi.
-Hadithi inahusu mapenzi ya Sela na Masazu.
-Mwandishi anaturudisha nyuma mahali ambapo Masazu na Sela walikutana.
2.Maswali ya balagha.
-Mamake Sela anamuuliza babake Sela kwani Sela si msiba wao bali wa mamake tu.
-Masazu anauliza Sela kwa nini hakujikinga.
3.Taswira.
-Hii ni picha ya mawazoni.
-Hii inajitokeza ambapo Masazu anakichomeka kidole chake ardhini akiwasilisha kiapo kwa Sela kuwa mapenzi yake ni ya dhati.
4.Taluki.
-Hali ya kutojua kilichotendeka hapo mbeleni.
-Ambalo Sela na mtotowe wanatumbukia majini.
-Wakati ambapo Masazu aliapa kiapo aliyeyusha nafsi ya Sela na hatukwambiwa nini ilitendeka.
5.Sadfa.
-Haya ni mambo ambayo hayakutarajiwa kutendeka.
-Sela na Masazu walioana hata baada ya Masazu kumsaliti.

MBINU ZA LUGHA


1.TASHBIHI

Hulinganisha kitu na kingine k.m;
·        Kiwiliwili chake mithili ya mbwa anayekabiliana na chatu macho kwa macho.
·        Ulimwengu wake ulivurugika, akawa kama tiara inayopeperushwa na upepo ikaendaarijoyo.
·        Nafasi kama hiyo hutokea kwa nadra ya jua kupatwa na chui aliyelivizia windo lake na sasa limetokea, akajiandaa.

2. Tashhisi

Sifa ya kukipa kitu chenye hakina uhai( uhaishi)
·        Mambo haya mawili yalielekeaa kuungana kuhujumu mkakati wao.
·        Matone yalitua sehemu yao ya hujuma. Mwandishi arejelea pale ambapo Sela na Masazu walikuwa wamejificha chini ya mwembe.
·        Mabaki yalielekea kutapika wanafunzi wakikena kiume.

3.Semi.
·        ….baridi shadidi ya usiku(uk59)ina maana kuwa huo ulikuwa na baridi kali.
·        Alijaribu kuvuta kumbukumbu(uk59)yaani alianza kukumbuka.
4.Methali.
·        Mimba ile ya Masazu ilikuwa kanda la usufi.Methali hii inasema kuwa mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi.
·        Uchungu wa mwana aujuaye mzazi.(uk63)
5.Istiara.
·        Nyumbani mwa Butali kuligeuka kuwa jehanamu.
·        Mimba ya Sela inalinganishwa na msiba.
·        Usiku wa giza-kukosa matumaini.






               
SHAKA YA MAMBO.
 Hadithi hii inamhusu msichana  wa miaka 29 hivi.Tunampata asubuhi na mapema akiwa mwenye gari la abiria akielekea kazini.Anapata gari limejaa lakini kijana mmoja anamwondokea kiti ili akae,jambo lisilo la kawaida hasa hapa Afrika.Akiwa njiani anawaza mengi kuhusu maisha yake.Anaona kuwa tangu afike Nairobi hajapata yale mambo mawili aliyoyafuata kujifunza usekritari na kuwa na uhuru.
Alikuwa anaishi na mzee Mwinyi  na familia yake katika mtaa wa Madaraka Estate alipokuwa amekodisha nyumba.Mzee huyu alimchukua kama mwanawe.Pia alikuwa na rafiki wa kiume aliyeitwa Kamata.Hatimaye anafika kazini,mkahawa uliokuwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa J.K.I.A na kuanza kazi.Mkubwa wake Grace hangeweza kushika zamu yake kwa sababu alikuwa na miadi yake lakini angemlipa baadaye.Kamata alifanya ya kukagua ya wasafiri humo uwanjani.
Tunamuona mzungu mteja akiacha bunda la noti za dola ya Kimarekani  zaidi ya alfu moja.Esther anachukua na kushindwa atazipeleka wapi.Kisha Kamata na Grace wanaingia na kuanza kuchukua  zile dola Kamata akidai kuwa atampa mwenyewe pesa.Ajabu ni kuwa Kamata hakumwona yule mzungu tena.Angemjuaje?Kisha Esther na Kamata  walikuwa wakisuhubiana.Esther akawaza kuwa Kamata hawezi mjua abiria huyo kwani hakumweleza wasifu wake.

Maudhui.
                              Ni adhali ya maisha ya mjini hasa kwa vijana watafutao kazi.
Kazi.
Tunamuona Esther akielekea Nairobi kutafuta kazi.

Unafiki.
Kamata anajifanya mwema na kuchukua zile pesa na hajui anayempelekea.

Uaminifu
Esther anaaminika kwa kazi yake.

Elimu.
Esther amesoma na bado anataka kuendeleza masomo.

Shaka(kukosa uhakika)
Esther anashaka kuwa Kamata atarudisha zile pesa.

6 .Usasa na mabadiliko.
Zamani wanawake hawakuelimishwa  lakini swala hili limeingia ambapo Kamata anampisha Esther kiti kwenye gari.

7.Uajibikaji.
Esther aliwajibika kazini mwake.

8.Uvumilivu.
Esther anavumilia akidhani atabadilishwa zamu.

9.Usaliti.
Grace  anamsaliti Esther kwa kuwa na uhusiano na Kamata.

Wahusika.
1.Esther.
-Ni mhusika mkuu.
-Ametoka Machakos.
-Anafanya kazi ya hoteli J.K.I.A
-Anaishi kwa mzee mwinyi.

Sifa.
1.Mwajibikaji.
Aliajibika kwa kazi yake katika hoteli.
2.Mshamba.
Anadanganywa kwa rahisi sana. 

3.Mvumilivu.
Alisubiri ili abadilishwe zamu.

4.Mwoga.
Hakutaka kuambia Kamata anampenda.

5.Mwenye shaka.
Alishaka kwa vile pesa zitamfikia yule mzungu.
6.Mwadilifu.
Hajiingizi katika mapenzi ya nje ya ndoa.
7.Mwenye mapenzi ya dhati.
Anampenda Kamata.
8.Mwaminifu.
-Alipopata zile dola alimrejeshea mteja.
-Anashawishika kwa urahisi.

2.Kamata.
-Ni mfanyikazi katika uwanja wa J.K.I.A
-Ni rafikiye Grace.
-Anapenda starehe na anasa.
Sifa.
1.Ndumakuwili.
-Ana uhusiano na Grace na Esther.
2.Mlaghai.
Anamdanganya Esther.
3.Msaliti.
Anamsaliti Esther mapenzi yake.
4.Hana subira.
Aliona gari la Esther limekaa na kuingia kwa Grace.

3.Grace.
-Ni rafikiye Kamata.
-Ni mkubwa wa Esther kazini.

Sifa.
1.Mpenda anasa.
Anaenda vilabuni kisiri na Kamata.
2.Msaliti.
Anamsaliti Esther.
3.Mwenye tamaa.
Anatamani bunda lile na dola la mzungu.
4.Msiri.
Hakumweleza Esther  wanaenda na nani.
5.Mwongo.
Wana uhusiano na Kamata na kumdanganya ya Esther kuwa hawana uhusiano na Kamata.
MBINU ZA LUGHA.
1.Maswali ya balagha.
Kuna maswali ya kuchochea hisia na ambayo hayana majibu.kwa mfano.
Esther anapokuwa kazini anawaza sana kumhusu Kamata.Anajiuliza maswali ya balagha kama Kamata kweli anamjali naye huyu pia anashughulika kutafuta pesa.
2.Utohozi.
Baadhi ya maneno ya kizungu yametamkwa kama ya Kiswahili.km kompyuta-computer,disko-disco,blauzi-blouse.
3.Mbinu rejeshi.
Inatumika katika (uk4) ambapo mwandishi anaturudisha nyuma katika maisha ya babake Esther.
4.Tashhisi.
Hali ya kuvipa vitu visivyo hai sifa za vitu vyenye uhai.



NDOA YA SAMANI





Hadithi hii inasimuliwa katika nafsi ya kwanza.Mwandishi amechukua nafasi ya mhusika mkuu,Abu na kumtumia kusimulia.Hadithi inaanza kwa kisegere nyuma.Mbele kwa sababu msimulizi anaanza kwa sehemu inayopaswa kuwa ndiyo ya mwisho wa hadithi.
Abu anaeleza kuhusu harusi iliyokuwa ikifanyika kati yake na Amani.Mwanzoni Abu alitaka kumuoa Amali lakini kwa kuwa alikuwa maskini wazazi wa amali wakakataa.Baadaye alipata kazi ya uhamali Arabuni na kuweza kujiwekea akiba iliyomsaidia kuanzisha biashara ya uchukuzi  wa abiria na kutajirika sana.
Kwa kuwa  hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na msichana yeyote,marafiki zake walimshauri  amrudie Amali wake.Abu alirudi kwa akina Amani ili kumposa tena safari hii lakini wazazi wa Amali hawakumkatalia posa yake hasa kama ilivyokuwa desturi yao.Wazazi wa Amali walimshauri Amali  aagize kununuliwa zawadi tele na za bei ghali na Abu.
Ikawa pia harusi sharti ifanyiwe nyumbani mwa Amali na tena iwe kukata na shoka.Siku ya arusi ilipofika kila kitu kilikuwa shwari lakini Abu alikataa kushiriki katika awa hii na hivyo basi arusi ikavunjiliwa bali.Abu alisihi kuwa Amali hakumpenda yeye bali aliyapenda mali aliyonayo sababu ya Abu kufikiri hivi ni kuwa sababu Amali alikuwa amemkataa alipokuwa maskini.Harusi iliyotarajiwa haikutendeka bali iliwaacha watu vinywa wazi. 
Dhamira.
Ndoa  yapaswa kujengwa katika msingi wa mapenzi si wa mali.Mwandishi anataka kutufundisha kuwa ndoa nzuri si ya pesa.

Maudhui.
1.Ndoa.
Msimulizi alimtaka Amali amwoe lakini kulikuwa na katizi kwa upande wa mvulana kwa kuwa hakuwa na pesa.Inatufunza usiolewe kwa sababu ya mali.Ndoa iwe ni maamuzi ya wenye kuoana.
2.Umaskini.
Msimulizi alikuwa ametoka kwenye familia ya kupigiwa mfano.Mwandishi anazingatia swala la umaskini lisiwe zingitiki kwa mapenzi.
2.Tamaa.
Mamake Amali alikuwa na tama ya kutajirika ndio maana alimkataa mwandishi mwanzoni.
4.Kisasi.
Msimulizi alilipiza kisasi kwa kukataa kumwoa Amali kwa vile yeye alikahaliwa mwanzoni.
5.Usaliti.
Amali alisalitiwa na msimulizi aliyemtoroka siku ya arusi.Mamake Amali alimsaliti mwandishi kwa kumkataza mwanzoni aoe Amali.Pia alimsaliti Amali kwa kumkataza aolewe na mwandishi.
6.Changamoto.
Mwandishi anapitia mambo magumu .mfano;Umaskini,kukosa kazi na pia kukataliwa na mamake Amali.
7.Bidii.
Mwandishi  alienda Arabuni na kujikaza na kuwa tajiri.
8.Utajiri.
Mamake Amali anataka kutajirika.

Wahusika.
1.Mwandishi.
Ni mhusika wa kiume anayopitia mambo magumu maishani.
Sifa.
1.Mchochole.
Kwao walikuwa maskini wa kupigiwa mfano.
2.Mwenye bidii.
Alipopata uajiri Arubani, alitia bidii na kutajirika na kuweza kujenga nyumba yake pamoja nay a wazazi wake.
3.Msaliti.
Alimsaliti Amali kwa kukosa kumuoa.
4.Mwenye kisasi.
Alikataa kumuoa Amali kwa vile alikataliwa hapo zamani kumwoa na Mamake Amali kwa kuwa hakuna na pesa.
5.Mkarimu.
Aliitikia kununua vitu ambavyo alivyopendekezwa kununulia familia yake Amali ili amuoe.Pia aliwatafutia ndugu zake kazi huko Arabuni.
2.Amali.
Msichana aliyetakiwa kuolewa na msimulizi.
Sifa.
1.Mtawa.
Anakaa kwao nyumbani na kutojishughulisha kwenda kufanya mapenzi kiholela.
2.Mtiifu.
Anawatii wazazi wake na pia dini yake.
3.Mrembo.
Wengi walimtaka kwa sababu ya urembo mwandishi aliyesoma.
4.Mtamaduni.
Alifuata mambo ya kitamaduni.
3.Wazazi wa Amali.
(i)Mamake.
Sifa.
1.Mwenye tamaa.
Anaitisha mahali ya bintiye ili atajirike.
2.Mwenye ubinafsi.
Anajiitishia vitu vyake pekee kama mahari ili Amali aolewe.
Mtindo wa lugha.
Ametumia misemo .kwa mfano;
Kupata jiko-kuoa
Walalahai-tajiri
Walalahoi-maskini
Maskini hohehahe-umaskini



MIZIZI NA MATAWI


Hadithi hii inatusimulia kisa cha mvulana mmoja kwa jina lake Sudi.Alilelewa na mama tajiri aliyemsomesha hadi chuo kikuu na mwishowe akaajiriwa.Alizoea kuuliza kama alikuwa na babake mzazi tangu utotoni akajulizwa kuwa babake mzazi ni Abdalla lakini hajawahi muona.
Siku moja alimuuliza mamake aliyetengeneza hadithi ya uongo kuwa Abdalla alimkimbia akiwa bado hajamzaa Sudi.Jioni moja Sudi akitoka stareheni zake alikutana na mwanamke mmoja aliyemwomba usaidizi.Alimpeleka  hadi kwao na kumwajiri kama yaya.Bibi huyu alimsimulia  Bi.Mkubwa jinsi alivyomtupa mtoto kwenye pupa la taka kwa kukosa uwezo wa kumlea.
Baadaye Bi.Mkubwa alimweleza Sudi kuwa mamake mzazi ni yule mfanyikazi wake na kuomba wasameheane.
Dhamira.
Hadithi hii inatufunza kuwa hata mtu akipotelewa na waliokaribu naye ama wakose kumsaidia bado anaweza kuendelea na kufaulu maishani.
Maudhui.
1.Mapenzi.
Sudi alipendwa na wasichana wawili Radhia na Waridi.Wasichana wengine pia walimpenda  Sudi kwa  utanashati wake.
2.Ukatili.
Bi.Kudura alifanya ukatili kwa kumtupa mwanawe kwenye pipa la takataka.Alijua hili lilikuwa kama kuua lakini hakujali.
3.Majuto.
Bi.Kudura anajuta kwa kumtupa mwanawe na baadaye hakuweza kupata mtoto aliomba Mola amsamehe.
4.Uana haramu/malezi.
Sudi hakumjua babake jambo lililomsumbua sana kimawazo.
Alimuomba mamake amwambie ukweli lakini alimdanganya.
5.Elimu.
Licha ya kuwa mwanaharamu,Sudi alisomeshwa na mamake hadi kiwango cha juu hadi akawa daktari.
6.Anasa.
Sudi alipokuwa ulaya alihudhuria sherehe iliyokuwa ya kukata na shoka ambayo ilikuwa ni sikukuu ya pasaka.Kulikuwa na muziki na wanawake wengi walitaka kucheza na Sudi.Pia alimpeleka mpenziwe Radhia kustarehe huko.
WAHUSIKA.
1.Sudi Abdalla.
(a)Mtana shati.
Ni kijana aliyependa usafi sana kwani tunamwona akijikwatua alipokuwa akijiandaa kwenda karamuni.
(b)Mkarimu.
Mara kwa mara alimpata Bi.Kudura njiani na hakumpita .Alimpa msaada aliotaka.
(c)Mwenye heshima.
Aliwaheshimu mamake na Bi.Kudura .Licha ya kuwa Bi.Kudura alikuwa maskini mwombaji,Sudi alimwita kwa majina ya heshima.Pia hakuwahi kumtuma amletee chochote.
(d)Mwenye utu.
Kutokana na utu wakealimsaidia Bi.Kudura.Alimwonea huruma alipompata njiani karibu na makaburi.
(e)Anapenda anasa.
Anapenda kuhudhuria karamuni na sherehe na mpenziwe Radhia.
(f)Mwenye mapenzi ya dhati.
Alimpenda sana mamake na Radhia mpenziwe na kufanya uchumba naye.

2.Bi Mkubwa.
Huyu ndiye aliyemwokoa Sudi alipotupwa kwenye pipa la takataka na mamake mzazi.Alimlea kama mwanaye.
Sifa zake.
1.Ni mwongo.
Alimdanganya Sudi kuwa yeye ndiye mamake mzazi  na kuwa babake alikuwa akiitwa Abdalla lakini alikufa na kumwachia mamake ulezi.
2.Ni mkarimu.
Bi.Kudura alipopelekwa kwake alikubali kukaa naye na hata akampa vitu alivyoagizwa na Sudi.
3.Ni msiri.
Aliweza kuiweka siri juu ya asili ya Sudi kwa muda mrefu tangu Sudi akiwa mtoto.
4.Mwenye mapenzi ya dhati.
Bi Mkubwa alimpenda Sudi na kumlea kama mwanaye.
5.Msamehevu.
Alimsamehe Bi.Kudura naye akasamehewa na Sudi.

3.Bi.Kudura.
Huyu ndiye aliyemzaa Sudi nje ya ndoa na kumtupa kwenye pipa la takataka kwa sababu aliona aibu.
Sifa zake.
(a)Ni mkatili.
Alifanya ukatili kwa kumtupa mtoto mchanga kwani hakujua kama angeokotwa na mtu au angeliwa na mnyama.
(b)Ni mnyenyekevu.
Kwa sababu ya hali yake ya umaskini alinyenyekea ili asaidiwe.
(c)Ni mcha mungu.
Alijua kuwa tendo la kumtupa mwanawe ilikuwa dhambi kwa mungu.

MBINU ZA SANAA NA LUGHA.
1.Taharuki.
Sudi alikuwa na hamu ya kumjua babake mzazi.Naye mamake alimweka na taharuki kwa muda mrefu.
2.Methali
-Mungu akikupa kilema hukupa na mwendo.Sudi alitaka mamake amwambie ukweli ndipo ajue jinsi ya kuishi na ukweli huo.
-……yaliyopita huwa yamepita.Sudi alitaka kuyasahau maisha ya anasa aliyoishi alipokuwa ulaya.
-Kuvyaa kupona.Mwanamke anapopata mtoto,mtoto huyo atakuja kumfaa baadaye akiwa mkubwa.
-Damu ni nzito kuliko maji.Bi.Kudura aliongozwa na kudura hadi ilipo damu yake na kumpata mwanawe Sudi.
3.Misemo.
-Kata tama-kosa matumaini.
-Tulia kama maji ya mtungi-tulia sana.
-Piga gari moto-Gurumisha gari.
-Walikuwa hawajijui hawajitambui-hawajiwezi.
-Piga moyo konde-Amua kufanya jambo.
4.Maswali ya balagha.
-Furaha yangu itoke wapi tena?
-Kuna ukatili gani zaidi ya huo?
5.Kuchanganya ndimi.
Kwa mfano:Handsome,Tea breeze,Royal palm.
6.Uzungumzi nafsia.
Sudi alijisemea mwenyewe anaposema.’Kumbe ni kweli  wanavyoniita’Sudi alisaini kimoyomoyo.
7.Tashhisi.
Gari unahaishwa tunapoambiwa kuwa Sudi alipiga gari lake moto na taratibu likatambaa na kuanza masafa kuelekea lilikokusudiwa.
8.Jazanda.
Kwa Sudi maneno haya yalikuwa msumeno unaokeketa kwa maumivu makti.
9.Tashbihi.
…..lakini ulimi wangu mzito kama nanga.
10.Mbinu rejeshi.
Sudi anaturejesha nyuma huko ulaya  alipokuwa akisomea na kutuonyesha jinsi maisha yalivyokuwa.
11.Sadfa.
Kukutana kwa Sudi na Bi. Kudura ilikuwa sadfa kwani hakutarajiwa.
12.Utohozi.
Hoteli-hotel
Bia-beer
Muziki-music
Benki-bank
Densi-dance
 13.Nidaa.
Sudi alikuwa akitabasamu-tabasamu ya fahari kwa uzuri wake.
Alifariki ghafla na kuniacha na mimba yako,tena changa!
Ikawa kama mtu aliyefundua tandu akafundika nge.
Naam,watu walikuwa wawiliwawili…ndume na mke!
Alimrudi  kila mmoja alikuwa na ulimwengu wake.
Inanikumbusha kauli ya wahenga …kuvyaa kupona!
Aa vile nao na umetulia! Hapo kabsa!

1 comment:

  1. FairPlay Casino: online casinos with live dealer
    FairPlay Casino Online is an online casino in which หารายได้เสริม players can choose from 5 different 인카지노 slot games 메리트카지노 including blackjack, roulette,

    ReplyDelete