SAMAKI WA NCHI ZA JOTO
Hadithi hii anaanzi wakati ambapo wahusika
Zac na Christine wamo chumbani mwa Zac
wakipga gumzo. Chumba hicho kilikuwa na picha ya bob marley
ilityorarukararuka juu ya dawati la zac
Pindi tu
Peter ambaye ni rafikiye Zac aliingia. Peter alikuwa muuza samaki wan chi za
Joto nje ya nchi hii. Christine alitabasamu kwa geresha alipomona Peter
aliyeonekena kuvutiwa na chumba uchwara cha Zac. Zac aliyependa sana kuongea
kama Mmarekani,alimkaribisha Peter kitini lakini alikataa kukikalia alikalia
kitanda ambapo Christine alikuwa ameketi, Christne alijivuta mbali naye.
Zac alimwelezea Peter kuwa Christine ni
rafiki ya na akawaletea vinywaji. Wakati huo alivunja kimya kilichokuwa
chumbani humo na kumwongelesha Christine. Alimuuliza kosi aliyokuwa anasomea
naye akajibu akiwa ametabasamu. Baada ya muda mfupi Zac alirudi nyumbani na
Christine akamaliza kinywaji chake na kuwaaga alipokuwa njiani alikashifu nafsi
yake mbona hakusema jambo lolote la maana.
Mwishoni mwa juma Zac alimwambia Christine
kwamba Peter angetaka amtembelee tena kwani alipendezwa naye na pia anaweza
enda na rafikiye Miriam Peter aliishi huko Tank hill.
Siku ilipowaadia Peter aliwaandalia vinywaji
huku wakipga gumzo walitazama video ya ‘Karate kid’. Pindi tu video iliisha
Miriam aliongozwa katika chumba cha wageni naye Christine akapelekwa chumbani
mwa Peter na Zac akabaki kochini.
Naye Christine akawa na mazoea ya kwenda Tank
Hill. Dadake Christine Dorothy alimwonya Christine kuhusu uhusiano wake na
Peter lakini aliipuuza mawaidha ya dadake.
Christine alitaka kujua jina la pili la Peter
lakini alikataa kumwambia kwani alitaka kuheshimiwa huko Afrika, Baadaye alitambua kwamba jina lake ni Smithson na alitoka tabaka la
chini la wazungu.
Siku moja
Peter alimpigia simu Christine aende kwake na alipowasili walianza burudani na
baadaye alijipata kitandani mwa Peter . Baada ya miezi Christine aligundua
kwamba ni mja mzito na alijua kwamba
kama angemwambia Peter hangefanya lolote na kasha akaamua kuavya mimba.
Christine alienda kumweleza Peter,lakini wote hawakutaka mtoto. Christine
alitabiri gari iliyokuwa na muziki wenye mapigo ya juu na kuelekea nyumbani.
WAHUSIKA
·
Christine/ msimulizi
·
Zac
·
Peter
·
Deogracias na Wafanyakazi wa Peter
·
Miriam
·
Dorothy
·
Margaret
·
Jagjit na Sunjah Patel
CHRISTINE
Ni msimulizi wa hadithi ya Samaki wa
Nchi za Joto. Ni msichana wa wa umri wa miaka ishirini anayesomea Sosholojia
katika chuo Kikuu cha Makerere.
Anadhihirika kama mwenye sif
zifwatazo;
Kwanza ni msichana msomi kwa
sababu tunaelezwa kuwa alisoma hadi Chuo Kikuu. Zac anamueleza Peter kuwa
Christine ndiye msichana mrembo zaidi pale chuoni.
Christine anajitokeza kama mdadisi
wa mambo, anamchuja Peter na kumuumbua kimaumbile. Anadadisi na kuelewa
kuwa Peter alipata faida kubwa kutokana na biashara ya samaki. Samaki ambao
anadai kuwa wanarejeshwa na kuuzwa katika maduka ya nyama pendwa. Anang’amua
kuwa Peter na Zac walifanya biashara ya bangi.
Kila mara, anaichuja nafsi yake na
kujiuliza maswali, anajishutumu kwa kutomwambia Peter jambo la maana.
Anayachuja maneno na matendo ya watu kwa makini. Anajihakiki na kuyahakiki
matendo yake. Anaigundua japo anaikwepa hali yake ya umaaskini, kudhulumiwa na
kudharauliwa na Peter.
Ni mwepesi wa kushawishika.
Kutokana na udhaifu huu, Christine anajiingiza katika uhusiano na Peter.
Anashawishika kwa haraka kuandamana na Zac hadi kwa Peter. Anashawishiwa na
Margaret kuavya mimba. Kutokana na udhaifu huu, anatumiwa na kutupwa.
Unuhimu wa Christine
Ni kielelezo cha wasichana wenye
elimu na wajihi lakini wanaoponzwa na ulimwengu kutokana na umaskini na tama.
Isitoshe, Christine anawakilisha
dhulma inayofanyiwa wanawake na waafrika kwa ujumla.
Ni kana kwamba mwaandishi anamtumia
Christine kutuonya dhidi ya kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi kiholela
bila ya kizisikiliza nathari zetu. Matendo na hatma ya Christine inadhihirisha
ukweli wa methali, ‘Enga kabla ya kulenga’ / ‘Tahadhari kabla ya hatari’ /
‘Usipoziba ufa utajenga ukuta’ na nyingine nyingi zenye maana sawa na hiyo
Hatimaye, baada yake kutumiwa na
kutupwa na Peter, Christine anaamua kurjea kwao pengine akiongozwa na imani
kuwa, ‘Mwenda tezi na omo, marejeo ni ngamani’
Maisha ya Christine
yanatudhihirishia namna wazungu wanapozitumia raslimali za Afrika na
kuzizorotesha kabla ya kuzitupilia mbali.
ZAC
Ni mwanachuo mwenza wa Christine,
hivi tunaweza sema kuwa yeye ni msomi. Aidha, Peter ni mwenye bidii kwa
sababu tunaelezwa kuwa wakati wa likizo, yeye alikuwa akifanya kazi katika
kampuni ya Peter.
Anaelezwa na Christine kama kijana
aliye na uhalisia, kwamba tofauti na vijana wengine, Zac hakuwa na ndoto
za kiuwendawazimu za kuwa watu wakubwa maishani.
Zac anajitokeza kama mwaafrika aliyekengeuka.
Anajidhihirisha kama mwafrika anayeiga kuzungumza kwa wamarekani.
Zac ni mshawishi na ndiyo
sababu anatumiwa na Peter ili kumshawishi Christine akubali kwenda Tank Hill.
Katika ushawishi huu, anajitokeza kama mpenda anasa, anamwambia
Christine; … utafurahia matembezi hayo sana, patakuwa na vinywaji vyakula
tele na video… (uk 30)
Pia, Zac anajitokeza kama kijana
mlevi kwa sababu anapokuwa nyumbani mwa Peter, analewa na kuanza
kubwabwaja.
Shughuli zake na Peter
zinamdhihirisha kama kijana msiri kwa sababu anajihusisha na shughuli za
kuuza bangi bila kutuhumiwa na yeyote.
Umuhimu wa Zac
Zac ni kielelezo cha cha waafrika vibaraka
wanaoiga mienendo ya kimagharibi bila kuichuja. Pia, anawaakilisha wafrika
wachache wanaotumiwa na wageni kulichafua bara la Afrika kupitia kwa dawa za
kulevya na usherati. Zac ni wakala wa peter anayetumiwa kuyapenyeza maovu
barani.
Kupitia kwa mhusika Zac, maudhui ya
ukoloni mamboleo, ukengeushi, umaskini, usaliti na matumizi ya dawa za kulevya
yanaelezeaka.
PETER
Huyu ni mwanamume wa kizungu mwenye
umri wa yapata miaka thelathini na tano. Yeye ni mlanguzi wa dawa za kulevya
japo anajificha katika biashara ya ununuzi na uuzaji wa samaki. Hivyo anaweza
kuelezwa kama mnafiki. Unafiki wake pia unajitokeza pale anapozungumza
na Christine kwa upole wakiwa katika chumba cha Zac, (uk 29) upole huu
unatoweka pindi tu anapotua mguu afisini pake.
Aidha, Peter ana madharau kwa
waafrika. Anawadharau kwa kutoiandika busara inayodaiwa kuibwa kutoka Misri.
Anadharau desturi za waafrika na kumbusu Christine shavuni tena kadamnasi ya
watu. Pia, anawapa wafanyakazi wake kazi ngumu na kuwaamuru kama nyapara.
Umuhimu wa Peter
Peter ametumiwa kuendeleza maudhui
ya ukoloni mamboleo yeye ni mzungu anayeendeleza uozo katika jamii ya kiafrika;
Anapunja raslimali ya Afrika kama vile samaki. Anachangia matumizi ya dawa za
kulevya, anawaingiza vijana katika ulevi na anasa huku akiwafanya wasahau
masomo yao, anawatumia wasichana waafrika kimapenzi na kuwatupa pindi
anapomaliza kukidhi haja yake. Isitoshe anahujumu uchumi wa nchi kwa kushiriki
biashara ya magendo ya kuuza na kununua sarafu.
Kwa ujumla, matendo ya Peter
yanazorotesha uchumi na maadili ya Afrika.
Shughuli zake ni kioo cha
kutuonyesha chanzo cha umaskini, upotovu wa kimaadili na unyonge wa watu wa
Afrika.
Kupitia kwa mhusika Peter,
tunang’amua ukweli wa methali kuwa, ‘vyote ving’aavyo si dhahabu’
DEOGRACIAS NA WAFANYAKAZI WENGINE WA
PETER
Deogracias ni mfanyakazi wa Peter wa
nyumbani. Mbali naye, pana wafanyakazi wengine afisini pa Peter.
Kwa jumla, wafanyakazi wa Peter ni watiifu,
wanamhudumia bwana wao vyema. Aidha, wafanyakazi wa Peter ni waoga. Deogacias
anauvumilia uovu utendwao na Peter kwa wasichana wa kiafrika badala ya kuulani.
Wafanyakazi wengine wanajitia kufanya kazi Peter anapowatazama.
Umuhimu wa wafanyakazi wa Peter
Wafanyakazi hawa wanaashiria unyonge
wa mwaafrika. Unyonge huu umetokana na kubebeshwa mzigo mzito wa kuwatumikia
mabwana wa kizungu. Inahuzunisha kuwa wafanyakazi hawa hawafanyi juhudi zozote
za kujikomboa.
MIRIAM
Na rafikiye Christine, anaelezeka
kama msichana mrembo. Anaelezwa na Christine kama msichana mrefu
na mwembamba, mwenye macho ya vikombe Aidha, Miriam ana ujasiri
wa kuvuta sigara na kulewa kadamnasi ya watu. Kwa mintarafu hii basi tunaweza
kuhitimisha kuwa Miriam amepotoka kimaadili. Utovu wake wa nidhamu
unaendelea kudhihirika wakati ambapo yeye pamoja na Margaret wanaunga mkono azma
ya Christine ya kuavya mimba
Ulevi wa Miriam unadhihiriika waziwazi wanapomgeni Peter. Analewa
na kuanza kucheka sebuleni kivoloya.
Umuhimu wa Miriam
Miriam anawakilisha wasomi
waliopotoka kimaadili kwa kujihusisha na uhuni kama vile uvutaji sigara, ulevi
na uavyaji mimba.
DOROTHY
Huyu ni dadake Christine mkubwa.
Anaelezwa kama mlokole, …Dorothy alikuwa mkristu aliyeokoka…(uk. 31)
Licha ya kuwa mkubwa wa Christine,
anakosa ujasiri wa kumkanya mnunawe dhidii ya kuhusiana na Peter. Badala yake,
Dorothy anadai kuwa aliota Christine akipewa sumu na wazungu.
Umuhimu wa Dorothy
Kupitia kwa Dorothy, tunapata
kufahamu madhara ya kutolikabili tatizo kwa ujasiri. Dorothy ni kielelezo cha
jamaa walioshindwa kutekeleza wajibu wa kuwashauri wadogo zao.
MARGARET
Ni dadake Miriam anayefanya kazi ya
uuguzi katika zahanati moja jiijini. Utovu wake wa maadili
unajitokeza pale anamuunga mkono Christine kuavya mimba. Anaitumia taaluma yake
vibaya kuwasaidia wasichana kuavya mimba.
Umuhimu wa Margaret
Anawakilisha wataalamu waliopotoka
kimaadili na wanaoongozwa na tama huku wakishirikiana kufanya maovu kama vile
uavyaji mimba
JAGJIT NA SUNJAH PATEL
Hawa ni wahindi waliofanya biashara
ya magendo na Peter. Mbali na kuwa wajanja wa kufanya biashara ya
magendo, wawili hawa nii watu laghai kwa kuwa wanapania kumuuzia Peter
noti bandia
Umuhimu wa Jagjit na Sunjah
Hawa wametumiwa kama wahusika
wajenzi kwa sababu wanaijenga tabia ya kiulaghai ya Peter. Pamoja na Peter,
wanaendeleza hujma dhidi ya uchumi wa nchi.
MASWALI
‘Msimulizi hampendi Peter kwa
dhati’, jadili ukirejelea hadithi fupi ya Samaki wa Nchi za Joto.
Jadili uhusika wa Miriam, Dorothy na
Margaret katika ujenzi wa wahusika wakuu kwenye hadithi.
DHAMIRA
Yamkini hadithi imelenga kujadili
uovu unaoingizwa katika nchi za bara la Afrika na wazungu. Uovu huu ni pamoja
na ulevi, ukahaba, ulanguzi wa dawa za kulevya, biashara ya magendo na ukahaba.
Azma hii mbi inachangiwa na uwepo wa waafrika wasaliti kama Zac, waoga kama
wafanyakazi wa Peter, wasio na msimamo thabiti kama Christine na wale wasio na
ukakamavu kama Dorothy.
Margaret na mtaalamu wa unusukaputi
ni baadhi ya wataalamu ambao wanatumia maarifa yao na taluma zao kuangamiza
jamii badala ya kuiimarisha.
Msimamo wa mwandishi; Japo mwandishi anaelekea kuyahusisha matatizo ya Afrika na
wageni, anasisitiza mchango wa waafrika wenyewe katika kujizorotesha.
MASWALI
Je,ni nini suala kuu katika hadithi?
MAUDHUI
Mafunzo yafwatayo yanajitokeza
katika hadithi fupi ya Samaki wa Nchi za Joto
Ukoloni mamboleo; Peter anawafanyisha kazi wafanyakazi wake naa kuwatolea
amri kama nyapara. Aidha, anawanyanyasa wasichana wa kiafrika kimapenzi.
Aidha biashara ya Peter ya samaki ni
ya kujinufaisha yeye binafsi huku akiwapunja waafrika.
Pia, anawatumia vijana kama Zac kwa
manufaa yake ya kibinafsi
Usaliti; Zac anausaliti urafiki wake na Christine kwa kumuongoza
kuingia katika urafiki na Peter. Licha ya kujua tabia za Peter, Zac
anamshawishi Christine kuingia katika urafiki naye.
Vilevile, Christine anazisaliti
hisia zake. Ni bayana kuwa hisia za Chrisine zinamuonya dhidi ya kujiingiza
katika urafiki na Peter. Hata hivyo anazipuuza na kujitia katika urafiki
uliomsababishia madhara tele.
Mapenzi; mapenzi yanayojitokeza katika hadithi yametawaliwa na
unafiki na usaliti.
Zac anajifanya rafiki wa Christine
lakini hatimaye anamsaliti kwa kumtaka ashiriki mapenzi na Peter.
Peter naye ana mapenzi ya uongo kwa
Christine. Anajifanya kama mwenye kumjali lakini Christine anaposhika mimba na
kuavya anampuuza na kumtupa. Inaelekea kuwa alimpenda tu kwa muda ili kukidhi
haja yake ya muda.
Yamkini Christina naye anampenda
Peter kutokana na dhifa kedekede alizoandaliwa pamoja na zawadi mbalimbali
alizompa.
Ulanguzi na Matumizi ya dawa za
kulevya; maudhui haya yanaendelezwa na
Peter pamoja na Zac. Tunaelezwa kuwa Zac alimtafutia Peter bangi.
Ukengeushi; huku ni kupotoka na kutenda mmbo kinyume na matarajio ya
jamii. Zac ndiye mhusika aliyekengeuka sana.
Anajitia kutaka kuzungumza kama
mmarekani mweusi. Pia, hataki kuzungumza Kiganda na Deogracias, badala yake,
yeye anazungumza Kiingereza.
Tabia ya Miriam kulewa na kuvuta
sigara kadamnasi ya watu haitarajiwi katika jamii ya Afrika.
Aidha, suala la kupigana busu
hadharani halikubaliwi na jamii ya afrika. Hivi basi, Christine anakengeushwa
na mienendo ya Peter ya kumbusu hadharani.
MASWALI
Eleza namna maudhui
Utabaka, Elimu, Ubarakala na
ulaghai, Matatizo ya wanawake
DAMU NYEUSI
Ni hadithi inayomhusu Fikirini ambaye ni mwanafunzi wa shahada ya
Uzamifu aliyeenda kusomea Marekani. Huko uzunguni anakutana na changamoto za
kubaguliwa kwa rangi ya na wazungu na weusi wenzake.
Hadithi iaanzapo anaachwa na basi ambalo
linaendeshwa na mzungu kwa kushukiwa
kuwa jambazi. Hatimaye anakumbuka
alivyofikishwa mahakamani na kupigwa faini baada ya kuitwa plisi na
mwanamke mzungu aliposahau kufunga zipu
ya suruali yak. Aliona kwamba kama angekuwa Afrika,ndugu zake wangemfanyia
hisani badala ya kumwitaia polisi. Jaji mweusi
alimtoza faini ya dola mia mbili na kuepuka kifungo cha miezi sita
gerezani.
Baadaye alipokuwa akitembea kuelekea shuleni,alipatana na mwanamke mweusi ambaye alimwalika nyumbani
mwake. Fikirini hakujua nia yake lakini mwanamke huyo alikuwa amemweleza kuwa
atampeleka hadi chuoni lakini kwanza waingie nyumbani mwake.Wakiwa humo ndani,
ndugu yake mwanamke huyo aliufunga mlango.Fiona alianza kumwitisha pesa alizo
nazo lakini hakuwa nazo. Alijaribu kutoroka alipohisi kwamba yumo hatarini
lakini Fiona alimwita Bob na kumweleza kwamba Fikirini alikuwa anajaribu
kumbaka. Bob alimwambia Fikirini auwachilie mkoba wake naye Fiona kamwambia
avue nguo zote. Baada ya kuchakurachakura mifuko yake na kupata hamna kitu, Bob
alimwachilia na kumwambia asirudi huko tena. Fiona alikataa aachiliwe na kudai
kuwa angetaka kumuua. Hatimaye, Fikirini aliachiliwa huru akiwa tupu na
akakimbia kama mtu aliyepagawa.
Ijapokuwa Fikirini aliviacha vitu vyake
nyuma,kama vitambulisho,alimshukuru
Mungu kwa kumwachia uhai wake.
DHAMIRA
Mwandishi
anazungumzia kuhusu ubaguzi kati ya wazungu na weusi na pia weusi na weusi.
Dhamira ni kuwa mwandishi anakashifu swala la ubaguzi wa rangi.
MAUDHUI
1.UBAGUZI WA RANGI.
Watu wenye rangi nyeusi wanabaguliwa na
wazungu au weusi wenzao.Anabaguliwa barabarani kuwa yeye ni jambazi.
Pia chuoni
anabaguliwa.Anapewa alama chache ingawa anafanya vizuri katika mtihani. Weusi
wenzaka wanabagua kwa vile ametoka Afrika na ameenda kuwaharibia.
2.ELIMU.
Fikirini
alienda huko kutafuta elimu ambapo alikuwa anasomea shahada ya uzamiifu.
3.UJAMBAZI
Fikirini alikutana na majambazi wawili
aliowaita ndugu zake lakini walimvamia
na kumtupa nje akiwa tupu.
4.UVUMILIVU.
Fikirini aliweza kuvumilia matatizo mengi
kama ubaguzi ili awezekumaliza masomo yake na kurejea nyumbani.
5.USALITI.
“Dadake” Fikirini aliisaliti imani
yake kwa kumhadaa.
6.UKATILI.
“Dadake”
Fikirini alikuwa anataka kummaliza Fikirini kwa sababu ya kukosa pesa.
7.UNAFIKI.
Huyo “dadake” alijifanya mwema ili amsaidie
Fikirini lakini alikuwa na nia yake.
WAHUSIKA.
1.FIKIRINI.
Ni
mwanafunzi na ametoka katika nchi za Afrika.
SIFA
Ø Ni
mvumilivu,amevumilia ubaguzi;baridi na dhuluma
Ø Ni msomi,alienda uingereza ili aweze
kumalizia masomo yake ya shahada
Ø Ni mwoga,alijisaidia aliposhikwa na
woga
Ø Mwenye imani,aliamini kwamba Fiona
angeweza kumsaidia kwa gari lake nzee ili ampeleke chuoni.
Ø Mpole,alipoulizwa maswali ya upuzi
wenzake alivumilia
Ø Mwenye bahati mbaya (mdubira),alisahau
kufunga zipu ,alipatana na majambazi.
Ø Mjinga,aliamini kwa haraka kwamba
“dadake” angemsaidia.
Ø Mzalendo,aliipenda nchi yake.
2.WAZUNGU.
SIFA
Ø Ni wenye ubaguzi mwingi .
Ø Ni wenye imani potovu,wanaamini
kwamba Waafrika ni kama nyani.
3.FIONA NA BOB.
Ni
wamarekani weusi.
Ø
SIFA
Ø Ni majambazi.
Ø Ni wakatili,badala ya kumsaidia mtu
akiwa na shida wanazidisha
Ø Fiona ni mnafiki,alijifanya kumsaidia
Fikirini ila ana zake.
MTINDO
1.USIMULIZI
Masimulizi
ya mwandishi yanatumia nafsi ya tatu
2.KUCHANGANYA NDIMI.
Fikirini aliulizwa“Do
youspeak English?”“ someone called to say you are exposing yourself.”
“How
you doing?”
“Am cool” “I
say remove your clothes or else” “
I say shoot him Bob”
MATUMIZI YA LUGHA.
1.METHALI.
Ø Nyumbani ni
nyumbani ingawa ni pangoni - Ilitumiwa na Fikrini alipokuwa
akirejelea kwao nyumbani ambako ni Afrika naye ako uingereza ambako ni kuzurui
kuliko kwao lakini hata kama kwao si kuzuri ivo ni nyumbani.
Ø Baharia wa pemba hufa maji mazoea -
mabaharia wa Pemba wamezoea kufa mali na ni jambo la kawaida.
Ø Simba akikosa nyama hukula nyasi –
Fikirini alikosa chakula kizuri cha kukula kwa hivyo alilizimishwa kula chakula
chao.
Ø Siku ya kufa nyani miti yote huteleza
– Siku ya mkosi ni mkosi na hakuna jinsi
ambavyo mtu anaweza kuepuka.
2. TANAKALI ZA SAUTI
Pepesuka pepesu
pepesu.
Ø Nyapia nyapu nyapu
Ø Nyeupe pepepe
3.MISEMO
Ø Mlevi chakari – mtu aliyelewa
kupindukia .
Ø Maji yamezidi unga – mambo kuzidi
matarajio
Ø Kusalimu amri – kukubali.
Ø Kufa ganzi – kupoteza fahamu
Ø Elewa fika.
Heko! kazi nzuri.
ReplyDeleteHongera waandishi wetu twajivunia kuwa nanyi
ReplyDelete